• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

TAWJA chaanza kutoa elimu kwa majaji,mahakimu

by bajeti
November 17, 2022
in Habari
0
TAWJA chaanza kutoa elimu kwa majaji,mahakimu

Rais Samia Suluhu Hassan akizundua Kitabu cha Mwongozo wa Mashauri kwa Majaji na Mahakimu Oktoba 2022 jijini Dar es Salaam.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MIRIAM SARAKIKYA,ARUSHA

CHAMA cha Majaji na Mahakimu Wanawake Tanzania (TAWJA) kimeanza kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na   Rais Samia Suluhu Hassan  wakati wa  uzinduzi wa Kitabu  cha Mwongozo wa Mashauri kwa Majaji na Mahakimu kuhusu elimu ilyokuwa katika kitabu hicho.

Rais Samia alitoa maelekezo hayo Oktoba 20,2022 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akizindua kitabu hicho na kuagiza Majaji na Mahakimu nchini kutumia kitabu cha Mwongozo wa Mashauri kwa Majaji na Mahakimu kuhusu mashauri yanayohusu ukatili wa kijinsia kama moja ya miongozo katika usikilizaji wa mashauri ya aina hiyo.

Rais Samia amesema kitabu hicho kitawapa Majaji na Mahakimu wanaosikiliza mashauri yanayohusu ukatili wa kijinsia ujasiri wa kutoa uamuzi wa mashauri hayo ambao pia utawezesha kuachwa kwa mila, desturi na imani potofu zinazokandamiza na kupora haki za makundi  maalumu katika jamii ya watanzania.

“Katika kipindi cha Uongozi wangu nitahakikisha ninajenga nchi inayozingatia na kuheshimu misingi ya utawala wa sheria, haki za binadamu, na utawala bora kwa maendeleo ya nchi kiuchumi, kisiasa na kijamii”, amesema Rais Samia. 

Akizungumza  jijini Arusha Oktoba 13,2022 wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya wakufunzi wa kitabu hicho,Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ,Joachim Tiganga amesema kuzinduliwa kwa mafunzo hayo  ni ishara ya mipango iliyopangwa kwa umahiri na viongozi hao ili kuhakikisha kitabu hicho kinafundisha haki,mikataba ya kimataifa na haki  za binadamu.

Jaji Tiganga amebainisha kuwa, kitabu hicho kitainufaisha jamii nzima  kupitia maudhui  yaliyoandikwa huku walengwa  wakuu wakiwa ni  wanawake na watoto.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TAWJA,Joaquine De-Mello amebainisha  kuwa, wanaopatiwa  mafunzo hayo wataenda  kuwa  walimu wa  wenzao ili elimu hiyo  iweze  kutumika kikamilifu katika utoaji  wa  haki  katika utekelezaji  wa majukumu yao.

Amesema kuwa,wanaopatiwa mafunzo hayo ni  majaji na mahakimu ambao watasambaa nchi nzima kwa ajili ya kutoa elimu hiyo kuhusu kile kilichopo  kwenye kitabu hicho ikiwemo masuala ya haki za wanawake na watoto  pamoja na utekelezaji   wa mikataba ya  kimataifa  na haki za binadamu.

Kwa upande wake Katibu wa TAWJA ,Anipha Mwingira  amebainisha kitabu hicho  kitawasaidia  majaji na mahakimu kukitumia  kama rejea katika kutoa maamuzi  katika kesi ambazo watakuwa wanashughulikia.

Aidha amefafanua kuwa washiriki hao watapeleka  elimu hiyo katika mikoa  mbalimbali nchini  katika kufanya rejea kuhusu  masuala ya haki za ndoa,mirathi ,haki za  kibinadamu na kesi zingine mbalimbali .

 

Next Post
Wanajeshi wa Kenya wawasili DRC kukabiliana na waasi

Wanajeshi wa Kenya wawasili DRC kukabiliana na waasi

Serikali:Mpango wa Uchumi wa Bluu utasaidia mapambano athari za mabadiliko ya tabianchi

Serikali:Mpango wa Uchumi wa Bluu utasaidia mapambano athari za mabadiliko ya tabianchi

Wasimamizi vyombo vya habari vya China,Afrika wakutana Kenya

Wasimamizi vyombo vya habari vya China,Afrika wakutana Kenya

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In