• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Saturday, May 2, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Wanajeshi wa Kenya wawasili DRC kukabiliana na waasi

by bajeti
November 17, 2022
in Habari
0
Wanajeshi wa Kenya wawasili DRC kukabiliana na waasi

Wanajeshi wa Kenya

Share on FacebookShare on Twitter

KINSHASA,DRC

KUNDI la pili la wanajeshi wa Kenya wamewasili katika eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) lililoathiriwa na machafuko na hujuma za waasi ili kudumisha amani cha baada ya Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kukubaliana kupelekwa kwa vikosi vya kikanda.

Wanajeshi hao ambao walitoka Nairobi Mji Mkuu wa Kenya na kusafiri hadi katika Mji wa Goma ni sehemu ya wanajeshi wa Kenya zaidi ya 900 ambao watakuwa nchini DRC ambapo watajiunga na wanajeshi kutoka nchi nyingine wanachama wa EAC ili kuisaidia serikali ya Kinshasa katika mapambano dhidi ya waasi ambao sasa wanadhibiti maeneo muhimu na hivyo kupelekea maelfu ya raia wa nchi hiyo kukimbia makazi yao.

Kamanda wa Kikosi cha Wanajeshi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Meja Jenerali Jeff Nyaga ameweka wazi malengo makuu mawili ya kikosi hicho huko Kongo katika mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema kama ninavyomnukuu:

“Tupo hapa kuulinda uwanja wa ndege wa kimataifa wa Goma dhidi ya hujuma yoyote, pamoja na makao makuu ya kikosi chetu huku michakato mingine ikiendelea.” amesema Meja Jenerali Nyaga

Kamanda Nyaga amebainisha kuwa vita haileti amani bali diplomasia inapasa kutafutwa na suala muhimu jingine linalopasa kuzingatiwa ni kuhusu kuyapokonya silaha makundi ya wanamgambo na kuyarudisha uraiani.

“Hatuwalengi waasi wa kundi la M23 pekee kwa sababu tunaona pande zote zimejielekeza kwa kundi hilo bali kuna makundi ya wanamgambo wanaobeba silaha mashariki mwa Kongo zaidi ya 120, na makundi hayo yamechochea kwa kiasi kikubwa ukosefu wa usalama katika eneo hilo. Iwapo michakato miwili hii itafeli, basi tutangia moja kwa moja katika njia ya tatu ambayo ni hatua ya kijeshi.” amesema Meja Jenerali Nyaga

Mwezi Juni,2022 Viongozi wa Jumuia ya Afrika Mashariki alikubaliana kupelekwa kwa kikosi cha kikanda huko Goma,DRC ili kukabiliana na makundi ya waasi wakiwemo M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda wakiwa wametekea maeneo makubwa huku wakiwa kilomita 20 kutoka mji wa Goma

Next Post
Serikali:Mpango wa Uchumi wa Bluu utasaidia mapambano athari za mabadiliko ya tabianchi

Serikali:Mpango wa Uchumi wa Bluu utasaidia mapambano athari za mabadiliko ya tabianchi

Wasimamizi vyombo vya habari vya China,Afrika wakutana Kenya

Wasimamizi vyombo vya habari vya China,Afrika wakutana Kenya

Serikali yazitaka nchi za SADC kudhibiti   uchomaji holela wa taka unaosababisha  sumu ya uPOPs

Serikali yazitaka nchi za SADC kudhibiti uchomaji holela wa taka unaosababisha sumu ya uPOPs

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:8
  • Today's page views 8
  • Total visitors 16,033
  • Total page views 18,191

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In