• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Serikali yazitaka nchi za SADC kudhibiti uchomaji holela wa taka unaosababisha sumu ya uPOPs

by bajeti
November 22, 2022
in Mazingira
0
Serikali yazitaka nchi za SADC kudhibiti   uchomaji holela wa taka unaosababisha  sumu ya uPOPs

Viongozi kutoka Nchi za Jumuia ya Kusini mwa Afrika (SADC) zinatekeleza Mradi wa Kupunguza Uzalishaji wa Kemikali Sumu aina ya uPOPs wakiwa katika picha ya pamoja jijini Dar es Salaam Novemba 21,2022 mara baada ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mary Maganga kufungua warsha yao.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

KATIBU Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mary Maganga amezitaka nchi za Jumuia ya Kusini mwa Afrika (SADC) kuchukua hatua za kupunguza uchomaji holela wa taka ili kuhifadhi mazingira.

Nchi hizo zinatekeleza Mradi wa Kupunguza Uzalishaji wa Kemikali Sumu aina ya uPOPs zinadumu kwenye mazingira kwa muda mrefu kutokana na uchomaji holela wa taka.

Maganga ametoa wito huo Novemba 21,2022 jijini Dar es Salaam wakati akifungua warsha kwa  nchi  za SADC ambazo zinazotekeleza mradi huo.

Hata hivyo,Maganga alizitaka nchi hizo kuhakikisha zinafikia malengo yaliyowekwa ya utekelezaji wa mradi huo kwa kuhuisha taarifa muhimu za kikanda zinazohusu uchomaji holela wa taka kwa kuwa na kanzidata.

Maganga amefafanua kuwa  wananchi wa mataifa wanufaika wa mradi wanapaswa kuelimishwa kuhusu madhara yatokanayo na uchomaji holela wa taka na hatua zinazochukuliwa na kila nchi katika kukabiliana na athari zitokanazo na uchomaji holela wa taka.

“Malengo ya mafunzo katika warsha hii ni kukuza uelewa na ujuzi kwa washiriki kuhusu kupunguza na kudhibiti uchomaji holela wa taka pamoja na hatua za kutatua changamoto za usimamizi wa kemikali nchini na kuweka malengo ya pamoja ya kupunguza uzalishaji wa kemikali aina ya uPOPs,” amesema Maganga.

Warsha hiyo inahusisha washiriki kutoka nchi saba wananchama wa SADC zinazotekeleza mradi huo ambazo ni Botswana, Eswatini, Lesotho, Madagascar, Msumbiji, Tanzania na Zambia.

Next Post

Makamishna wa Tume za Uchaguzi kutoka nchi tisa wakutana Dar es Salaam

Dkt.Mpango awataka wataalamu,wawekezaji kujadili rasilimali za fukwe kuongeza mchango wake kiuchumi

Dkt.Mpango awataka wataalamu,wawekezaji kujadili rasilimali za fukwe kuongeza mchango wake kiuchumi

Jeshi la EAC kuwasambaratisha waasi wa M23

Jeshi la EAC kuwasambaratisha waasi wa M23

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In