HARARE,ZIMBABWE
SERIKALI ya Zimbabwe imepitisha Muswada wa Sheria ya kuwaadhibu wananchi wasio wazalendo, ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na vikwazo vya kiuchumi dhidi ya taifa hilo la kusini mwa Afrika.
Waziri wa Habari wa Zimbabwe, Monica Mutsvangwa aliwaambia waandishi wa habari Novemba 24,2022 jijini Harare kuwa, Baraza la Mawaziri la nchi hiyo limepitisha muswada wa sheria hiyo inayokusudia kuwaadhibu Wazimbabwe wanaohujumu maslahi ya taifa hilo.
Sheria hiyo itakayojulikana kama “Sheria ya Uzalendo’ itawaadhibu wananchi wa Zimbabwe wanaoeneza taarifa kwa nchi za Magharibi ili ziiwekee vikwazo nchi hiyo.
Aidha sheria hiyo inataka adhabu ya lazima kwa watu wanaopatikana na hatia katika kesi za ubakaji na mauaji, na pia imetoa tafsiri pana zaidi ya ‘mihadarati hatari’ mbali na kurekebisha kipengele kinachozungumzia jinai ya matumizi mabaya ya ofisi (mamlaka).
Hata hivyo vyama vya kisiasa nchini humo vimepinga sheria hiyo na kuitaja kuwa ya kifashisti na inayokanyaga katiba ya nchi.
Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) mara kwa mara imekuwa ikitoa mwito wa kuondolewa haraka na bila masharti yoyote vikwazo dhidi ya Serikali ya Zimbabwe.
Vikwazo hivyo vilivyowekwa mwaka 2002 na Marekani, Uingereza na Umoja wa Ulaya, ambavyo ni pamoja na vizuizi vya kibiashara na kifedha, vimeikwamisha Zimbabwe kuboresha uchumi wake na ustawi endelevu




Discussion about this post