• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Mradi wa LDSF wasaidia wananchi kumiliki ardhi

by bajeti
November 26, 2022
in Mazingira
0
Mradi wa LDSF wasaidia wananchi kumiliki ardhi

Baadhi ya Wananchi wa vijiji vya Haubi na Mafai wilayani Kondoa mkoani Dodoma wakishiriki hafla ya kukabidhi hati miliki za kimila ambazo zimetolewa na Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais chini ya Mradi wa Kurejesha Ardhi iliyoharibika na Kuongeza Usalama wa Chakula katika Maeneo kame nchini (LDSF) Novemba 25,2022(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

SERIKALI imekabidhi hati miliki za kimila 305 kwa wananchi wa vijiji vya Haubi na Mafai wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kurejesha Ardhi iliyoharibika na Kuongeza Usalama wa Chakula katika Maeneo kame nchini (LDSF).

Akikabidhi hati hizo Novemba 265,2022 wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya hiyo Dkt. Hamisi Mkanacha aliishukuru Ofisi ya Makamu wa Rais inayotekeleza mradi huo kwa ushirikiano na Tume ya Taifa ya Mipango na Matumizi ya Ardhi kwa kufanikisha zoezi hilo.

Amesema kupatikana kwa hati hizo ni fursha kubwa kwa wananchi wa vijiji hivyo na wilaya kwa ujumla kwani zitawasaidia kuepusha migogoro ya ardhi na kuwawezesha kupata mikopo kutoka kwenye taasisi za kifedha.

Hata hivyo, Dkt. Mkanacha amewataka wanufaika wa mradi huo kuheshimu matumizi ya ardhi yaliyopangwa na kuwa ni kosa kisheria kuitumia kwa namna nyingine.

Amewaagiza viongozi wa ngazi mbalimbali wilayani humo kusimamia kikamilifu mipango ya ardhi iliyowekwa ili wananchi wasiende kinyume na  kuibua migogoro.

“Ndugu zangu wananchi baadhi ya maeneo utakuta mnapanga matumzi ya ardhi lakini anatokea mtu mmoja mjuaji, mjanja anatafuta mteja anamuumizia ardhi, kwa hili tutakuwa wakali mno,” amesema Mkanacha.

Kwa upande wake Mratibu wa kitaifa wa Mradi wa LDFS Joseph Kihaule ameeleza kuwa  hati miliki za kimila zinazotolewa hazihamishiki na zinabaki kwa ndugu husika hivyo hairuhusiwi kuuzwa.

Aidha ameongeza kuwa mojawapo ya faida za hati hizo ni kuwa hazitalipiwa kodi ya mwaka kama ilivyo kwa hati zingine za mijini hivyo wananchi wana fursa ya kutumia ardhi hiyo kwa maendeleo endelevu.

Akizungumzia shughuli zingine za mradi huo,Kihaule amebainisha kuwa kwa sasa vijiji vya Haubi na Mafai vinatarajia kuchimbiwa visima ili kupunguza makali ya ukame unaokabili wilaya hiyo.

Vilevile shughuli zingine kupitia mradi huo ni kuundwa kwa vikundi vya uzalishaji mali ikiwemo ufugaji wa nyuki, mifugo pamoja na uchimbaji wa visima ambavyo vikikamilika vitatumika katika umwagiliaji.

 

Next Post
Dkt.Mpango:Viongozi wa dini  saidieni kulea vijana kimaadili ili Taifa liwe kwenye mikono salama

Dkt.Mpango:Viongozi wa dini saidieni kulea vijana kimaadili ili Taifa liwe kwenye mikono salama

TBA watakiwa kutekeleza miradi inayozingatia ubora na gharama nafuu

TBA watakiwa kutekeleza miradi inayozingatia ubora na gharama nafuu

CCM:Shahada ya Udaktari kwa Rais Samia ni matokeo ya kazi  kubwa aliyoifanya  kwa  watanzania

CCM:Shahada ya Udaktari kwa Rais Samia ni matokeo ya kazi kubwa aliyoifanya kwa watanzania

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In