• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

CCM:Shahada ya Udaktari kwa Rais Samia ni matokeo ya kazi kubwa aliyoifanya kwa watanzania

by bajeti
November 30, 2022
in Siasa
0
CCM:Shahada ya Udaktari kwa Rais Samia ni matokeo ya kazi  kubwa aliyoifanya  kwa  watanzania

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete akimtunuku Shahada ya Udaktari wa Falsafa wa Heshima ikiwa ni Shahada ya Udaktari wa Juu katika Humanitia na Sayansi Jamii Rais Samia Suluhu Hassan Novemba 30,2022 jijini Dar es Salaam.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Falsafa (Phd)ikisema hatua hiyo inadhihirisha na kusadifu kazi kubwa na anayoitekeleza kiongozi huyo mkuu wa nchi kwa watanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam leo Novemba 30,2022 na Chama hicho na kutiwa saini na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka imeeleza kuwa  kazi kubwa na nzuri inayofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia ni chachu ya kutolewa kwa Shahada hiyo.

“Tumeguswa na kufurahishwa na uamuzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)kumtunuku Shahada ya Udaktari wa Heshima Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan katika mahafali ya 52 duru ya 5 yaliyofanyika Novemba 30, 2022  katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

“Uamuzi huo ni uthibitisho wa dhahiri wa kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Serikali ya CCM ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Dk. Samia Suluhu Hassan katika kuleta ustawi wa maisha na maendeleo endelevu kwa nchi yetu,” imefafanua taarifa hiyo.

Aidha imeongeza kuwa kati ya kazi kubwa iliyofanyika na kutumika kumtunuku shahada hiyo ni pamoja na mageuzi ya kiuchumi, kuimarisha misingi ya demokrasia, utawala bora na kuleta maendeleo ya jamii.

“Ameleta furaha na tumaini jipya miongoni mwa wananchi. Yote hayo ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025 uliochagizwa na utashi wake wa kisiasa, ukomavu na umahiri alionao katika uongozi.

“Shahada hiyo ni fahari kwa Chama na Watanzania wote ikionyesha kuwa nchi ina Rais anayewajibika kwa maslahi ya wote na kwamba itampa moyo kuwa wananchi wanaona kazi nzuri anazozifanya kwa taifa hivyo kumpa ari na nguvu ya kuendelea kutekeleza wajibu wake”imebainisha taarifa hiyo

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimemtunuku Rais Samia Suluhu Hassan  Shahada ya Udaktari wa Falsafa katika mahafali ya 52 duru ya tano yaliyofanyika  jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete amemtunuku Shahada ya Udaktari wa Falsafa wa Heshima ikiwa ni Shahada ya Udaktari wa Juu katika Humanitia na Sayansi Jamii.

 

 

Next Post
Naigeria yaondoa kiingereza kufundishia shule za msingi

Naigeria yaondoa kiingereza kufundishia shule za msingi

Kigahe:Wafanyabiashara tumieni teknolojia mbadala kukabili mabadiliko ya tabia nchi

Kigahe:Wafanyabiashara tumieni teknolojia mbadala kukabili mabadiliko ya tabia nchi

Serikali yaanza kutatua mgogoro wa vijiji na hifadhi ya Wembere

Serikali yaanza kutatua mgogoro wa vijiji na hifadhi ya Wembere

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In