• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Naigeria yaondoa kiingereza kufundishia shule za msingi

by bajeti
December 2, 2022
in Habari
0
Naigeria yaondoa kiingereza kufundishia shule za msingi

Rais wa Naigeria Muhamadu Buhari

Share on FacebookShare on Twitter

ABUJA,NAIGERIA

WAZIRI wa Elimu wa Nigeria Adamu Adamu  ametangaza sera yenye lengo la kukuza ufundishaji wa wanafunzi wa shule za msingi nchini humo kwa kutumia lugha za ndani badala ya lugha ya Kiingereza.

Adamu  ameeleza kuwa, wanafunzi hujifunza vizuri zaidi pale wanapofunzwa kwa kutumia lugha yao mama.

Hata hivyo Waziri Adamu amekiri kuwa, kutekeleza sera hiyo mpya itakuwa na changamoto kwa sababu itahitaji kazi kubwa kuandaa nyenzo za kufundishia na kuwapata walimu ikiwemo  idadi ya lugha zinazozungumzwa katika nchi hiyo zinazofikia  zaidi ya 600.

Mpango huo uliopewa jina la” Sera ya Taifa ya Lugha”, tayari umepitishwa ili uanze kutekelezwa ambapo maelezo ya kufundisha wanafunzi kwa miaka sita ya kwanza katika shule za awali yatakuwa kwa lugha ya mama.

Hata hivyo, Kingereza ni lugha rasmi inayotumika nchini humo ambapo taasisi zote za kielimu hutumia lugha hiyo kama lugha ya kawaida ya kufundishia na kujifunza.

Pamoja na hayo bado haijafahamika ni lini serikali itaanza kutekeleza mfumo huo mpya wa kuachana na lugha ya Kiingereza katika shule za msingi.

 

Next Post
Kigahe:Wafanyabiashara tumieni teknolojia mbadala kukabili mabadiliko ya tabia nchi

Kigahe:Wafanyabiashara tumieni teknolojia mbadala kukabili mabadiliko ya tabia nchi

Serikali yaanza kutatua mgogoro wa vijiji na hifadhi ya Wembere

Serikali yaanza kutatua mgogoro wa vijiji na hifadhi ya Wembere

DODOMA

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In