• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

BRELA yashukuru vyombo vya habari ongezeko usajili wa makampuni

by bajeti
April 2, 2023
in Habari
0
BRELA yashukuru vyombo vya habari ongezeko usajili wa makampuni

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari mkoani Morogoro Machi 29,2025 juu ya ongezeko la usajili kwa makampuni ya watanzania kutokana na mchango wa wanahabari hao.(Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,MOROGORO

WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), imesema Kampuni za Kitanzania 13,663 zimesajiliwa sawa na ongezeko la asilimia 27 ikilinganishwa na Kampuni 10,790 zilizosajiliwa mwaka 2021.

Mbali na hilo lakini pia  Kampuni za Kigeni 93 zimesajiliwa sawa na ongezeko la asilimia 29 ikilinganishwa na Kampuni za kigeni 72 zilizosajiliwa mwaka 2021.

Takwimu hizo zimetolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa, wakati akizungumza katika mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) ulioanza  Machi 29,2023 Mjini Morogoro.

Nyaisa amewapongeza Wahariri wa Vyombo vya habari kwa mchango mkubwa wanaoutoa kwa BRELA katika kuwafikia wadau popote walipo kupitia vyombo vya habari na kueleza kuwa jitihada hizo zimesaidia kuongeza uelewa wa wadau kuhusu huduma zinazotolewa na BRELA.

“Nikiri kwamba, vyombo vya habari hasa ninyi Wahariri mmekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya BRELA, ambapo mmewezesha wafanyabiashara kutumia huduma zinatolewa na Wakala za kurasimisha biashara  na kupata ulinzi wa Miliki Ubunifu pamoja na Leseni.

“Hii imetokana na jitihada zenu za  kutoa habari mbalimbali zinazohusu BRELA bila vikwazo vyovyote”, amesema Nyaisa.

Aidha Nyaisa ameongeza kuwa  kupitia vyombo vya habari, wananchi wameelewa mifumo inayotumika kufanya sajili mbalimbali,

ikizingatiwa kwamba sajili zote zinafanyika kwa njia ya mtandao na kuchangia ongezeko la sajili na utoaji wa Leseni za Biashara kundi “A”.

Nyaisa ameitaja mifumo hiyo  kuwa ni pamoja na Mfumo wa Usajili kwa njia ya Mtandao (ORS) na Mfumo wa Tanzania National Business Portal (TNBP).

Kutokana na mafanikio hayo Nyaisa ameeleza kuwa kwa mwaka  2023 BRELA imepanga kukutana na Wahariri ili kujadili na kukubaliana namna bora ambayo itawezesha kushirikiana katika eneo la uwezeshaji wa biashara nchini na kudumisha zaidi uhusiano uliopo.

Akifafanua zaidi Nyaisa amebainisha kuwa kutokana na uelewa wa wananchi kuongezeka kumekuwa na  ongezeko la Sajili kwani katika kipindi cha miaka miwili yaani mwaka 2021 mpaka 2023, BRELA imeshuhudia ongezeko la idadi ya sajili za kibiashara na utoaji wa Leseni ambapo

Ameeleza kuwa Majina ya Biashara 25,507 yamesajiliwa ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 17 ikilinganishwa na Majina ya Biashara 21,836 yaliyosajiliwa mwaka 2021.

“Alama za Biashara na Huduma 3,607 zimesajiliwa ambazo ni sawa na ongezeko la asilimia 15 ikilinganishwa na Alama za Biashara na Huduma 3,137 zilizosajiliwa mwaka 2021.

“Pia kwa upande wa Leseni za Biashara kundi “A”  Leseni 13,663 zimetolewa ambazo ni sawa na ongezeko la asilimia 13 ikilinganishwa na Leseni 10,790 zilizotolewa mwaka 2021″amefafanua Nyaisa

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,Nape Mnauye (wa pili kushoto) akimkabidhi cheti cha shukrani Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Godfrey Nyaisa,wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Kitaaluma wa Wahariri wa Vyombo vya Habari (TEF), unaofanyika mjini Morogoro mACHI 29,2023.Kushoto nni Mwenyekiti wa TEF Deodatus Balile na katika ni Makamu Mwenyekiti TEF Bakari Machumu(Picha na mpigapicha wetu)

Mkutano wa 12 wa Mwaka wa Kitaaluma wa Wahariri unaofanyika kwa siku nne, umefunguliwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye  ukiwa na kaulimbiu ya “Sheria za Habari na Maendeleo ya Vyombo vya Habari”

Next Post
Kiwango cha kuzaliana chashuka Japan,yashuhudia watoto chini ya 800,000 wazaliwa kwa mwaka

Kiwango cha kuzaliana chashuka Japan,yashuhudia watoto chini ya 800,000 wazaliwa kwa mwaka

Ekari Milioni 5.2 za Misitu kurejeshwa  ifikapo 2030

Ekari Milioni 5.2 za Misitu kurejeshwa ifikapo 2030

Sayansi,Utafiti na Ubunifu vyasisitizwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050

Sayansi,Utafiti na Ubunifu vyasisitizwa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In