• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Mbunifu wa Kaboni ataka kushirikiana na WFP

by bajeti
April 10, 2023
in Habari
0
Mbunifu wa Kaboni  ataka kushirikiana na WFP

Mbunifu wa Kaboni kwa kutumia vifuu vya nazi Tuberius Mario akipeana mkono na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jijini Dodoma baada ya kutangazwa mshindi wa kwanza katika mashindano ya Sayansi na Teknolojia mwaka 2022.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

MTAFITI na Mbunifu wa Kaboni inayotokana na vifuu vya nazi  Tiberius Mario amesema kwa sasa ameomba fedha kutoka Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) ili aweze kufanya utafiti juu ya kaboni yake kutumika katika kilimo.

Hayo ameyasema Aprili 9,2023 wakati akizungumza na Bajeti juu ya matumizi ya Kaboni hiyo kutumika kuondoa sumu iliyopo katika ardhi inayotumika kwa kilimo ama itakuwa na madhara ikiwa itatumika au itasaidia.

Amesema Kaboni anayotengeneza ina uwezo wa kutumika kusafisha maji kwa kunyonya uchafu lakini pia kwa watumiaji wadogo wa dhahabu katika eneo la uchenjuaji madini hayo hivyo kutokana na hilo ameona ni muhimu kufanya utafiti katika suala zima la kilimo ikiwa inamadhara au inasaidia

“Kwa sasa hatuwezi kusema kama inafaida katika ardhi ya kilimo am hasara hadi tufanye utafiti wa kina na kujiridhisha ndio sasa tutoe matokeo na kuona nini cha kufanya lakini sasa bado.

“Tumetuma maombi kwa WFP lakini bado hawajatujibu na tunaendelea kusubiri ili tufanye utafiti ambao Kaboni yetu inaweza kutumika katika ardhi ya kilimo kwa kunyonya sumu ili mazao yaweze kukuwa katika  ardhi yenye virutubisho ama itakuwa na madhara katika ukuaji wa mimea”amesema Mario.

Mario ambaye ni mshindi kwa kwanza katika Mashindano ya Sayansi na Teknolojia maarufu kama (MAKISATU) yanayoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) mwaka 2022 amesema Kaboni yake imethibitishwa kwa asilimia 98 kufanya kazi inayotakiwa.

Aidha ameongeza kuwa kwa sasa baadhi ya makampuni makubwa ya uchimbaji dhahabu wameanza kuitumia Kaboni aliyoibuni kwa kutumia vifuu vya nazi katika kukamatishia madini ya hadhabu na wamethibitisha kuwa inafanya kazi nzuri.

Hata hivyo Mario amesema licha ya kusaidiwa na COSTECH kufika hapo alipofika lakini anahitaji kiasi cha Sh.Milioni 36 kufanikisha ndoto yake na kuwa na kiwanda kikubwa chenye uwezo wa kuzalisha maelfu ya tani za Kaboni ili zisiagizwe kutoka nje ya nchi.

Next Post
SHIVYAWATA washukuru mfumo wa walemavu wa miguu kuendesha gari

SHIVYAWATA washukuru mfumo wa walemavu wa miguu kuendesha gari

Mwanafunzi kidato cha kwanza atengeneza redio

Mwanafunzi kidato cha kwanza atengeneza redio

MUUNGANO

DODOMA

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:17
  • Today's page views 17
  • Total visitors 13,276
  • Total page views 15,024

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In