BEIJING,CHINA
CHINA imeendelea kukua kisayansi na teknolojia ambapo abiria nchini humo wataanza kulipia tiketi ya treni ya chini ya ardhi maarufu kama (Metro) jijini Beijing kwa kusanikisha (kuskani) kiganja cha mkono pekee.
Kampuni ya Metro ya jijini Beijing imetangaza kuwa imeanza kutoa huduma maalumu kwa abiria wake ya kuskani kwa muda mchache kiganja cha mkono ili kulipia nauli ya treni ya chini ya ardhi.
Huduma ya kuskani haraka kiganja cha mkono ni imeelezwa kuwa ni mwafaka zaidi kwa watu walio wazee kiumri,wenye matatizo ya kimwili na waliosahau kadi zao za Metro au wale ambao hawawezi kutumia simu za mkononi, ambapo wote hao wanaweza kulipia nauli ya usafiri huo kwa njia hiyo.
Huduma za malipo kwa njia ya kuskani kiganja cha mkono zimepangwa kutolewa katika Ofisi,Shule, Kumbi za michezo na migahawa kwenye maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.
China inaendelea kukuwa zaidi kiteknolojia za kisasa, katika kuboresha utoaji wa huduma katika vituo na maeneo ya umma.
Katika mwendelezo wa utoaji huduma hizo, mnamo mwaka 2022 baadhi ya njia za treni katika mji wa Shenzhen iilizindua mashine za kuskani sura ya mtu kwa ajili ya kulipia nauli ya metro; na mwaka huu, treni ya chini ya ardhi ya Beijing imezindua huduma hiyo kwa kutumia mfumo wa kuskani kiganja cha mkono




Discussion about this post