MOSCOW,URUSI
WIZARA ya Ulinzi ya Urusi imetangaza kuwa, jeshi la nchi hiyo limeshambulia na kuangamiza meli ya mwisho ya kivita ya Ukraine katika bandari ya Odesa.
Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la habari la IRNA lilinukuu taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Urusi ikisema kuwa, jeshi la anga la nchi hiyo limetumia silaha yenye shabaha ya hali ya juu kuteketeza meli ya mwisho ya kivita ya Ukraine ijulikanayo kwa jina la Yuri Olefirenko katika bandari ya Udesa ya kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Meli ya kivita ya Yuri Olefirenko ilitengenezwa nchini Urusi katika muongo wa 1990 lakini ilikuwa ikimilikiwa na Ukraine baada ya kusambaratika Umoja wa Kisovieti (USSR).
Meli hiyo imefanyiwa matengenezo kwa muda mrefu na matengenezo makubwa zaidi yalifayika mwaka 2016.
Wizara ya Ulinzi wa Urusi pia imesema katika taarifa yake hiyo kwamba, hivi sasa mapigano makali yanaendelea katika eneo la Avdeevka lililoko katika njia ya kuelekea kwenye jimbo la Donetsk.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa, idadi ya wanajeshi wa Ukraine waliouawa katika kipindi cha masaa 24 ya hadi wanatoa taarifa hiyo walikuwa 200.
Tangufebruari 24,2022,Urusi ilidai kuanzisha oparesheni ya kijeshi nchini Ukraine na miongoni mwa maeneo yanayolengwa sana na jeshi la Urusi ni ya majeshi ya anga na baharini ya Ukraine na kuangamiza zana na vifaa vya majeshi hayo.
Urusi inatumia manuwari zake za kijeshi na makombora yake ya kisasa kuangamiza maeneo ya kijeshi ya serikali ya Kyiv.




Discussion about this post