NA MWANDISHI WETU,DODOMA
SERIKALI imewaonya wafanyabiashara wachache wanaoendelea kuingiza, kuzalisha na kusambaza bidhaa za plastiki zisizokidhi viwango ambzo zinazotumika kama vifungashio na kusababisha uchafuzi wa mazingira katika maeneo mbalimbali nchini.
Akizungumza Juni 2, 2023 jijini Dodoma katika zoezi la usafi wa mazingira katika kuelekea kilele cha Siku ya Mazingira Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Juni 5 ya kila mwaka,Naibu Waziri wa Kilimo, Antony Mavunde amesema ni wajibu wa Wafanyabiashara kushirikiana na taasisi za Serikali katika kusimamia usitishaji wa Matumizi ya bidhaa za plastiki.
“Kumekuwa na juhudi mbalimbali za Serikali na wadau katika kukabiliana na uchafuzi wa mazingira utokanao na taka za plastiki, hata hivyo bado kuna ukiukwaji wa sheria kwa baadhi ya wafanyabiashara wanaoingiza na kuzalisha mifuko ya plastiki isiyokidhi viwango ambayo inayotumika madukani na watoa huduma” amesema Mavunde.
Hata hivyo Mavunde amewaka wananchi kuendelea kuiunga mkono Serikali katika kudhibiti matumizi ya mifuko na bidhaa za plastiki kwa kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali za mitaaa ili kurahisisha zoezi hilo la kutokomeza vifungashio visivyokidhi viwango ambavyo vimekuwa visambazwa kupitia njia za panya.
Aidha Mavunde amesema Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais imeendelea kufanya jitihada kubwa za kuhamasisha suala la utunzaji na uhifadhi wa mazingira katika maeneo ya miji mikuu nchini ikiwemo Jiji la Dodoma, hivyo ni wajibu wa wananchi wote nchinin kutosubiri Kilele cha Maadhimisho ya mazingira katika kujishughulisha na suala la usafi katika maeneo yao.
Awali akimkaribisha Mgeni rasmi, Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Switbert Mkama amesema katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani, Ofisi hiyo imejipanga kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma hatua inayolenga kupendezesha taswira ya Jiji hilo ambalo ni makao makuu ya Serikali.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Godwin Gondwe amesema Mkoa huo utaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuhakikisha kuwa Jiji la Dodoma ambalo ni Makao Makuu ya Serikali linaendelea kuwa safi.
Kilele cha Wiki ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambayo ina kauli mbiu isemayo “Pinga Uchafuzi wa Mazingira unaotokana na Taka za Plastiki”




Discussion about this post