LONDON,UINGEREZA
WATAFITI kutoka Chuo Kikuu cha Oxford nchini Uingereza wametoa matokeo ya utafiti walioufanya na kuonesha kuwa wanafunzi waliotumia maziwa ya mama zao wakiwa wachanga hupata alama bora zaidi katika shule za upili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa Juni 8,2023 na kituo cha habari cha parstoday.ir imeeleza kuwa kulingana na matokeo ya utafiti wa chuo hicho yameonesha kuwa wanafunzi ambao walinyonyeshwa kwa angalau miezi minne, wanapata kwa wastani, alama mbili hadi tatu zaidi kuliko wanafunzi ambao hawakunyonyeshwa na mama zao.
Mbali na hilo lakini pia, wanafunzi walionyonyeshwa kwa maziwa ya mama huwa wanafaulu masomo mengi zaidi na hivyo kufaulu zaidi kuingia vyuo vikuu.
Watafiti wa Chuo Kikuu cha Oxford wanasema kwamba walichunguza alama za kitaaluma za takribani wanafunzi 5,000 waliozaliwa kati ya 2000 na 2002 kwa muda mrefu ili kuchunguza uhusiano kati ya kunyonya mazima ya mama na alama zao za shule ya sekondari
Utafiti huo umeonesha kuwa, hata wakati masuala kama vile uwezo wa kiakili na hali ya kijamii na kiuchumi ya wanafunzi vilipozingatiwa, wanafunzi walionyonya mazima ya mama zao walikuwa na hali bora zaidi ya kimasomo na kitaaluma na walipata alama za juu katika shule za sekondari.
Mtaalamu kutoka taasisi ya Nuffield Department of Population Health Reneé Pereyra-Elías amesema kuwa mafanikio bora ya kielimu ni “moja tu” ya matokeo mazuri ya watoto wanaonyonya mazima ya mama zao, na kwamba maziwa ya mama yanapaswa kutolewa kwa mtoto kwa sababu husaidia “ustawi wa utambuzi” wa mtoto kwa kusaidia ukuaji wake wa neva.
Matokeo ya utafiti huu pia yamechapishwa katika jarida la “Archives of Disease in Childhood”.




Discussion about this post