NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar kimepokea kwa masikitiko na huzuni kubwa kufuatia taarifa ya kifo cha Kada,Mwanasiasa na Mfanyabiashara maarufu Mohamed Raza Hassanali aliyefariki Juni 08,2023 katika Hospitali ya Aghakan Jijini Dar es saalam.
Raza ambaye amewahi kuhudumu katika nafasi mbalimbali za ndani ya Chama na Serikali ikiwemo Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mkoa wa Kusini Unguja na Mshauri wa Rais wa Zanzibar katioka Serikali ya Awamu ya Tano katika masuala ya michezo.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolea Juni 8,2023 na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi –CCM ,Zanzibar Khamis Mbeto Khamis Makamu amesema Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi, ametoa salamu za pole kwa familia,ndugu,jamaa na marafiki,wanachama wa CCM na Watanzania wote walioguswa na msiba huo na kuwasihi waendelee kuwa na subira katika kipindi chote cha msiba huo.
“Enzi za uhai wake Mohamed Raza alikuwa ni kiongozi aliyelinda na kukipigania Chama chetu na alikuwa ni kada muadilifu,mchapakazi na mzalendo mwenye maono ya kimaendeleo ndani ya Chama na Serikalini”, amesema Makamu Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi.
Raza, alizaliwa Julai 08,1962 katika Mtaa wa Mkunazini Unguja, hadi ambapo hadi anafariki alikuwa ni Kada wa CCM na Mfanyabiashara mkubwa na amezikwa Juni 08,2023 katika Makaburi ya Kisutu jijini Dar es saalam.




Discussion about this post