OTTAWA,CANADA
SERIKALI ya Canada itaikabidhi Serikali ya Ukraine ndege ya mizigo aina ya Antonov-124, inayomilikiwa na shirika la ndege la Volga-Dnepr la Urusi baada ya kuishikilia tangu 2022.
Tangazo hilo linakuja huku kukiwa na ziara ya ghafla ya Waziri Mkuu wa nchi hiyo Justin Trudeau nchini Ukraine.
Kwa mujibu wa taarifa ya Waziri wa Uchukuzi wa Kanada Omar Alghabra aliyoitoa Juni 10,2023 amesema kuchukuliwa kwa mali hiyo muhimu ni hatua ya kwanza ya Serikali ya Kanada ya Sheria iliyoundwa na nchi hiyo ya kukamata na kutaifisha mali ambapo imeundwa ili kuweka shinikizo zaidi kwa Urusi.
Ndege hiyo aina ya An-124 Ruslan ilikuwa imekodishwa na serikali ya Kanada kutoka kwa shirika la ndege la Urusi kupeleka shehena ya vipimo vya Covid kutoka China mnamo mwaka 2022 na ilitua Toronto nchini humo Februari 27,2022 saa chache kabla ya nchi hiyo kufunga anga yake kwa ndege zote za Urusi,ambapo imekuwepo tangu wakati huo.
“Tangu mwanzo tumesimama upande wa watu wa Ukraine, na kutekeleza NOTAM dhidi ya ndege zote zinazomilikiwa na Urusi na zinazoendeshwa kwenda Kanada,”
“Tunasimama na Ukraine na tutachukua hatua zozote muhimu, ikiwa ni pamoja na utekaji nyara huu, kuweka shinikizo kwa Rais Putin.” amesema Alghabra.
Tangu Februari 2022, Kanada tayari imetoa kiasi cha dola bilioni 8 kusaidia vita vya serikali ya Kiev dhidi ya Moscow, huku ikiweka vikwazo vingi dhidi ya watu binafsi na mashirika ya Urusi.




Discussion about this post