• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Dkt.Mpango:Tanzania inaunga mkono jitihada za kuimarisha hali ya usalama Mashariki mwa DRC

by bajeti
July 11, 2023
in Habari
0
Dkt.Mpango:Tanzania inaunga mkono jitihada za kuimarisha hali ya usalama Mashariki mwa DRC

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Stargomena Tax (wa tatu kutoka kushoto), Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Innocent Bashungwa (wa tatu kutoka kulia) pamoja na wawakilishi wa vyombo vya ulinzi na usalama mara baada ya kushiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Utatu wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Organ Troika), Utatu wa SADC (SADC Troika) na nchi za SADC zinazochangia vikosi vya kijeshi katika nchi za Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo na Jamhuri ya Msumbiji. Mkutano huo umefanyika kwa njia ya mtandao Julai 11, 2023.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

SERIKALI ya Tanzania imesema inaunga mkono jitihada za kikanda za kuimarisha hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikiwemo Kaskazini mwa Jamhuri ya Msumbiji

Hata hivyo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo tayari kuchangia hali na mali katika misheni ya SAMIDRC ili kuhakikisha kanda inatimiza malengo yake

Hayo yameelezwa na Makamu wa Rais wa Dkt. Philip Mpango Julai 11,2023 wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Utatu wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC Organ Troika), Utatu wa SADC (SADC Troika) na nchi za SADC zinazochangia vikosi vya kijeshi katika nchi za Jamhuri ya Kidemkorasia ya Kongo na Jamhuri ya Msumbiji.

Mkutano huo ambao umefanyika kwa njia ya mtandao umelenga kuangazia hali ya usalama mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo pamoja na Kaskazini mwa Jamhuri ya Msumbiji.

Akizungumza katika Mkutano huo,Makamu wa Rais Dkt.Mpango amesema Tanzania inaunga mkono jitihada za kanda za kuimarisha hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Amesema analipongeza taifa hilo kwa utayari wake wa kutoa mchango wa ziada katika uanzishwaji wa Misheni ya SADC nchini humo (SAMIDRC).

“Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ipo tayari kuchangia hali na mali katika misheni ya SAMIDRC ili kuhakikisha kanda inatimiza malengo yake”amesema Dkt.Mpango

Katika hatua nyingine mkutano huo umeridhia kuongezwa kwa muda wa vikosi vya misheni ya SADC nchini Musumbiji (SAMIM) kwa miezi 12 kutoka Julai 16 2023.

Mkutano huo umehudhuriwa na marais nane kutoka nchi za Kusini mwa Afrika wakiwemo Rais wa Namibia Dkt. Hage Geingob, Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, Rais wa Malawi Dkt. Lazarus Chakwera, Rais wa Msumbiji Felipe Nyusi, Rais wa Zambia Hakainde Hichilema,

Marais wengine waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Rais wa Botswana Mokgweetsi Masisi, Rais wa Zimbabwe Dkt. Emmerson Mnangagwa, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi, Waziri Mkuu wa Lesotho Samuel Ntsokoane pamoja na Naibu Waziri Mkuu wa Angola Balozi Te’te Antònio.

 

Next Post
Demokrasia yaanza kuwashinda wamarekani

Demokrasia yaanza kuwashinda wamarekani

Bilioni 5.68 zatumika kuwalisha wahamiaji haramu

Bilioni 5.68 zatumika kuwalisha wahamiaji haramu

CCM yampongeza Rais Samia kuunda Wizara ya Mipango

CCM yampongeza Rais Samia kuunda Wizara ya Mipango

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In