• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Kaburi la ajabu lililoshindikana kuhamishwa

by bajeti
August 12, 2023
in Mazingira
0
Kaburi la ajabu lililoshindikana kuhamishwa

Kaburi la ajabu linalodaiwa kuwa ni Sharifu likiwa katikati ya Jiji la Dar es Salaam.(Picha na Goodluck Hongo)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

WAKAZI wa Jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania wameshangazwa na Kaburi la ajabu ambalo limeshindwa kuhamishwa huku likizungukwa na majengo marefu.

Kaburi hilo lililopo eneo la Posta katikati ya Jiji la Dar es salaam (maarufu kama Kaburi moja)  linadiwa kuwepo eneo hilo kwa zaidi ya miaka 70 iliyopita huku kukiwa na maelezo yanayochanganya kuhusu uwepo wake.

Hata hivyo Bajeti Communication ilimtafuta Afisa Habari wa Jiji la Dar es Salaam Tabu Shaibu kuelezea uwepo wa Kaburi hilo na sababu za kushindwa kuhamishwa katika eneo  la  bustani ya watu kupumzika.

Akizungumzia Kaburi hilo Shaibu alikiri kulifahamu na kueleza kuwa ni Kaburi la Sharifu “Nalifahamu ni Kaburi la Sharifu lakini kuna mhusika ambaye ni Afisa Utamaduni ndiye atakayekupa maelezo zaidi juu ya kaburi hilo”amesema Shaibu

Mmoja wa mafundi viatu katika eneo la Posta Saidi Mohamed amesema yeye analijua Kaburi hilo tangu miaka ya 1980 akiwa kijana mdogo  na hajui ni kwa nini limeshindwa kuondolewa.

“Ndilo Kaburi pekee katikati ya Jiji la Dar es Salaam na eneo lililopo ndipo watu wengi hukutana kama sehemu ya kijiwe maarufu kama ‘Kaburi Moja’ na eneo hilo miaka ya nyuma ndipo watu maarufu walikuwa wakikutana na kupanga mipango yao wakiwemo wanamuziki wa bendi mbalimbali za zamani “amesema Mohamed

Mohamed ameongeza kuwa katika jiji la Dar es Salaam kulikuwa na maeneo makubwa matatu ambayo watu maarufu walikuwa wakikutana kwa kuwa simu hazikuwa nyingi kama ilivyo sasa ambapo eneo la kwanza ambalo ukimtafuta mtu utampata yalikuwa ni  Posta,Kaburi Moja na Mnazi Mmoja ndio maaeneo maarufu kwa watu kukutana miaka ya nyuma na mipango yote hupangwa katika maeneo hayo.

Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wakiwa katika mazungumzo karibu na Kaburi hilo Julai 19,2023.

Kwa upande wake Aisha Seleman ambaye hukaa eneo hilo kusubiri kupata kazi amesema yeye awali alikuwa hajawahi kuliona Kaburi hilo lakini aliavyoanza kukaa hapo ndipo alipoliona na kushangaa kuwa katika eneo lenye pilikapili nyingi.

“Ninavyojua nasikia hili lilikuwa eneo la Msikiti sasa wakasema haiwezekani kujenga Msikini na Kaburi pembeni,waamue ujengwe Msikiti na Kaburi lihamishwe lakini kila walivyotaka kulihamisha ilishindikana,nasikia wamefanya kila linalowezekana kulihamisha imeshindikana ndio wakaamua kuliacha hadi sasa na Msikiti haukujengwa tena”amesema Seleman

Hata hivyo Seleman amebainisha kuwa kwa taarifa alizopata yeye ni kwamba vifaa vilivyotumika kuchimba ili kuliondoa Kaburi hilo vilivunjika vunjika huku wengine wakisema walipotaka kulihamisha walitoka nyuki.

Aidha Seleman ameongeza  kuwa baadhi ya watu hufika katika eneo hilo kuomba dua mbalimbali ,“ni eneo ambalo watu mbalimbali hufika wakiamini kuwa matatizo yao yataondolewa baada ya kuomba”amesema Seleman

Uchunguzi wa Bajeti Communication umegundua kuwa eneo lililo Kaburi hilo ni takribani hatua moja tu  kilipo kituo cha tax ambapo magari mengine hupaki jirani na kaburi hilo  huku viti vilivyojengwa kwa saruji vikizunguka bustani hiyo ya Kaburi Moja.

Bajeti Communication inaendelea kufuatilia zaidi kujua sababu za kutohamishwa kwa Kaburi hilo ndani ya eneo la bustani ambapo makumi ya watu hukaa eneo hilo kusubiri kazi na wengine kufanya biashara.

Next Post
Wafungwa 3252 ‘waigeuza jela nyumbani’

Wafungwa 3252 ‘waigeuza jela nyumbani’

Balozi Dkt.Slaa:Bila Muungano Zanzibar isingekuwa salama

Balozi Dkt.Slaa:Bila Muungano Zanzibar isingekuwa salama

Putin aionya Poland

Putin aionya Poland

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:6
  • Today's page views 6
  • Total visitors 13,062
  • Total page views 14,807

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In