MOSCOW,URUSI
RAIS wa Urusi Vladmir Putin ameionya Poland juu ya uamuzi wake kupeleka wanajeshi karibu na mpaka wa Belalus na kubainisha kuwa Moscow itajibu kwa njia zote vitisho juu ya mshirika wake mkuu Belarus
Kwa mujibu wa tovuti ya Serikali ya nchi hiyo ya RT ilimnukuu Kiongozi huyo wa Urusi Julai 21,2023 akisema kuwa viongozi wa Poland wanapanga kuunda muungano unaoungwa mkono na Jumuia ya Kujihami ya Nchi za Magharibi (NATO) ili kuingilia kati mzozo wa Ukraine na kutwaa baadhi ya maeneo ya magharibi mwa Ukraine pamoja na, pengine, Belarus,
Akizungumza katika Mkutano na Wajumbe wa Kudumu wa Baraza la Usalama la Urusi Julai 21,2023 jijini Moscow, Putin amesema serikali ya Kiev iko tayari kufanya lolote lile ili kusalia madarakani, ikiwa ni pamoja na kuuza watu wake na kukabidhi maeneo ya Ukraine kwa “wamiliki wa kigeni.”
Amesema wa kwanza katika mstari huo ni Wapolandi, ambao wanatarajia kuunda aina fulani ya muungano chini ya ‘mwavuli wa NATO’ na kuingilia moja kwa moja mgogoro wa Ukraine, ili ‘kung’oa’ kipande kikubwa zaidi cha ardhi na kurejesha kwao kama wanavyoaminikuwa maeneo yao ya kihistoria magharibi mwa Ukraine ya leo.
Akizungumzia ripoti ya Huduma ya Kijasusi ya Kigeni ya Urusi (SVR), Putin alipendekeza kwamba dhumuni la kweli la muungano kama huo lingekuwa tu kuchukua maeneo ya Ukrain.
“Matarajio ni dhahiri – ikiwa vitengo vya Poland vitaingia, kwa mfano, Lvov au maeneo mengine ya Ukraine, basi watabaki huko na watakaa humo milele.” na kuongeza kuwa inajulikana kwamba Warsaw inaota pia kudai sehemu za eneo la Belarusi.
Kiongozi huyo wa Urusi ameonya hata hivyo kwamba, wakati Ukraine ina haki ya kuuza sehemu kubwa ya eneo lake kama inavyotaka, linapokuja suala la Belarusi, uchokozi wowote dhidi ya sehemu ya Jimbo la Muungano utamaanisha uchokozi dhidi ya Urusi.
“Tutajibu hili kwa njia zote tulizo nazo,” amesema Rais Putin
Kwa upande wake Mkuu wa Huduma ya Kijasusi ya Kigeni ya Urusi (SVR), Sergei Naryshkin,amesema kuwa Warsaw ilikuwa ikifikiria kuteka maeneo ya magharibi ya Ukraine kwa kupeleka wanajeshi wake katika eneo hilo kama sehemu ya mpango wa usalama wa Poland-Lithuania-Ukreni.
Naryshkin amesema maafisa wa Poland wanafikia hatua kwa hatua kutambua kwamba “suala la kushindwa kwa Ukraine ni suala la muda tu,” bila kujali kiasi cha msaada wa kijeshi wa Magharibi uliotumwa kwa Kiev.




Discussion about this post