• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Magonjwa yanayowaathiri wanyamapori yatajwa

by bajeti
July 22, 2023
in Mazingira
0
Magonjwa yanayowaathiri  wanyamapori yatajwa

Ng'ombe pori maarufu kama Nyati(Mbogo)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK  HONGO

PAMOJA na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali dhidi ya kupambana na vitendo vya ujangili katika maeneo mbalimbali ya hifadhi na mapori ya akiba,wanyamapori pia wanakabiliwa na magonjwa mbalimbali yanayotishia uhai wao.

Akizungumza na Bajeti Communication jijini Dar es  Salaam,Kamishna Msaidizi kutoka Kanda ya Kusini Mashariki ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Keneth Sanga amesema kuna magonjwa mengi yanayowapata wanyamapori lakini yapo baadhi  ambayo yanayojulikana sana.

Amesema wanyamapori wanakabiliwa na Ugonjwa wa Miguu na Midomo (Foot and Mouth Disease) ambapo huo huwapata pia Ng’ombe, mbuzi na kondoo.

“Kichaa cha Mbwa (Rabies), huu ni ugonjwa unaowapata  pia jamii  ya Mbwa mfano Fisi na Mbwa Mwitu.

“Homa ya Nguruwe (African Swine fever) hii pia inawapata wanyamapori kama Ngiri na Nguruwe pori.

“Homa ya Bonde la Ufa (Rift Valley Fever) huu huwapata Wanyamapori jamii ya Ngo’mbe kama Nyati”amesema Kamishna Msaidizi Sanga

Kamishna Msaidizi Sanga ameongeza kuwa hayo ni magonjwa machache tu yanayowapata wanyamapori licha ya kuwa yapo mengi.

Hata hivyo kutokana na uvamizi wa njia za wanyamapori zinazowasaidia kuhama kutoka hifadhi moja hadi nyingine maarufu kama (Shoroba) kwa ajili ya kuzaliana na kutafuta malisho upo uwezekano wa magonjwa hayo kuwapata binadamu kutokana na makundi ya wanyama hao  kuingia na kuweka kambi katika makazi ya watu.

Aidha mabadiliko ya tabianchi ambayo husababisha mafuriko na ukame hupelekea  wanyamapori kuvamia makazi ya watu ili kutafuta chakula na maji hali ambayo pia inaweza kusambaza magonjwa hayo kwa binadamu na mifugo wanayoifuga.

Next Post
Kinana:Waliojaribu kuigawa nchi kwa misingi ya ukabila na udini wameshindwa

Kinana:Waliojaribu kuigawa nchi kwa misingi ya ukabila na udini wameshindwa

Matukio 1718 ya milipuko na moto hayajachunguzwa

Matukio 1718 ya milipuko na moto hayajachunguzwa

CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na  Shujaa wa Afrika,

CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na Shujaa wa Afrika,

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In