• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

Kinana:Waliojaribu kuigawa nchi kwa misingi ya ukabila na udini wameshindwa

by bajeti
July 23, 2023
in Siasa
0
Kinana:Waliojaribu kuigawa nchi kwa misingi ya ukabila na udini wameshindwa

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana akisalimiana na Viongozi wa Chama hicho Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma Julai 23,2023 mara baada ya kuwasilia kuanza ziara ya kikazi katika mikoa ya Manyara, Mara, Simiyu na Tabora (Picha na mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,DODOMA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdulrahaman Kinana,amesema kutokana na misingi imara iliyowekwa na waasisi wa Taifa,  watu waliojaribu kuigawa nchi kwa misingi ya udini ,ukabila,ubara na visiwani wameshindwa.

Hata hivyo amesema mafanikio makubwa yaliyofikiwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ndani ya miaka miwili ya uongozi wake yanatokana na utulivu, usikivu, kupokea ushauri na kufanya uamuzi wa busara kwa manufaa ya Watanzania.

Kinana ameyasema hayo leo Julai 23, 2023 alipokuwa qkiwahutubia wananchi wa Kondoa  mkoani Dodoma katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Kondoa Dk. Ashatu Kijaji kwa lengo la kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2023.

Amesema kuna watu wamejaribu kuwagawa kwa misingi ya ukabila wameshindwa, na kuna watu wamejaribu kuwagawa kwa misingi ya ubara na visiwani wameshindwa pia.

“Kuna watu wamejaribu kutugawa kwa misingi ya ukabila wameshindwa, kuna watu wamejaribu kutugawa kwa misingi ya ubara na visiwani wameshindwa,” amesema Kinana

Amebainisha kuwa kwa hali ilivyo na kwa hatua waliyopiga  mpaka kufika 2025 ana uhakika kila Mtanzania atakuwa na sababu ya kusema waendelee na CCM pamoja na Rais Samia Suluhu Hassan.

 “Hatusemi haya kwa kujivuna bali kwa utekelezaji wa Ilani ya CCM lakini tunaangalia na wenzetu wa nchi jirani wanakwendaje, Nchi yetu imetulia, inamaani, ina umoja, inamshikamano na malengo, na ina mipango ambayo inatekelezwa na kila mtu ni shahidi, CCM itaendelea kuchaguliwa kwa sababu ina sera nzuri ina Ilani nzuri inayotekelezeka,” amesema Kinana.

 

Makamu Mwenyekiti wa CCM Abdulrahman Kinana akisalimiana na wanachama chama hicho wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma Julai 23,2023 baada ya kuwasilia kuanza ziara ya kikazi katika mikoa ya Manyara, Mara, Simiyu na Tabora (Picha na mpigapicha wetu)

Wakati huo huo  Kinana, amewashauri viongozi wa CCM hicho katika ngazi zote kuendeleza umoja ili kwenda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 pamoja na Uchaguzi Mkuu mwaka 2025 wakiwa wamoja ili kuibuka washindi.

Kinana ameyasema hayo  wakati akizungumza na viongozi wa CCM katika kikao cha ndani cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.

“Napongeza kazi kubwa inayofanywa na viongozi wa CCM hususan katika ngazi kitongoji, Kijiji, mtaa na Kata kwa kazi nzuri mnayoifanya na mwakani ni mwaka wa uchaguzi, hivyo naamini wana CCM tutakwenda kwenye uchaguzi wa Serikali za Mtaa mwaka 2024 tukiwa kitu kimoja, tukifanya kampeni wamoja na tutaibuka na ushindi tukiwa wamoja, hivyo hivyo katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2025,” amesema Kinana.

Kinana amewasili mkoani Dodoma kuanza ziara katika mikoa ya Manyara, Mara, Simiyu na Tabora

Next Post
Matukio 1718 ya milipuko na moto hayajachunguzwa

Matukio 1718 ya milipuko na moto hayajachunguzwa

CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na  Shujaa wa Afrika,

CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na Shujaa wa Afrika,

Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In