• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

by bajeti
July 29, 2023
in Habari
0
Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

Balozi Dkt.Willibrod Slaa akizungumza na mwandsihi wa habari wa Bajeti Communication(hayupo pichani) nyumbani kwake jijini Dar es Salaam Julai 19,2023(Picha na Goodluck Hongo

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

BALOZI Mstaafu wa Tanzania nchini Sweden Dkt.Willibrod Slaa amesema kuwa hataacha kupiga kelele kutetea maslahi ya Taifa na kwamba katika suala la Bandari  hakuna  siasa.

Amesema tafsiri halisi ya siasa ni maisha,hivyo kama ni maisha basi kila mtu anafanya siasa kwa kuwa hata anayepanga bajeti ya familia yake kuhusu chakula naye anafanya siasa.

Balozi Mstaafu Slaa ametoa kauli hiyo hivi karibuni nyumbani kwake jijini Dar es Salaam wakati wa mahojiano maalum na mwandishi wa habari wa Bajeti Communication.

Amesema “Sisi hatupingi uwekezaji wowote ule na Tanzania tumewekeza miaka yote  tangu uhuru  kwani hata Arusha kuna mashamba makubwa ya maua na hela za Umoja wa Ulaya (EU) ndio zinafadhili mashamba hayo na huo ni uwekezaji na hakuna mtu anayepiga kelee”

“Tarehe Mosi Septemba nilitoa ahadi kuwa nimejitoa kwenye  vyama vya siasa yaani siasa za vyama nimeacha (Active Party Politics).

“Nikaahidi kwa maslahi ya Taifa langu sitaacha kupiga kelele ndio watu mnashangaa sasa mbona Dokta sasa unafanya siasa,hapana ni maslahi ya Taifa,katika suala la Bandari si suala la siasa, hapa hakuna siasa,hapa ni urithi wa watoto wetu na wajukuu watatulaani tuliachia,ni urithi wao.”amesema Dkt Slaa

Dkt Slaa ambaye pia licha ya kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden lakini pia aliwakilisha Nchi za  Nordic na Baltic  zikiwemo Finland na Denmark ameongeza kuwa kuna hela za Umoja wa Ulaya(EU) zinapanda  maua  kule Arusha na wako watanzania wamepewa hela na EU kwa ajili hiyo  kwani yeye alikuwa kwenye Bunge la pamoja na  EU na analifahamu hilo .

Amesema amekuwa mwakilishi wa Tanzania katika Bunge linaloitwa (Afrika,Carribean and Pacific Union (ACPU)(Bunge linalotokana na Mkataba wa Lome wa mwaka 1975) ambapo mwaka 1995 alipoingia bungeni alipata bahati ya kuingia kwenye Bunge hilo ambalo limeundwa kwa mujibu wa hicho kifungu cha Sheria ya Mkataba huo wa Lome ambao ni mji Mkuu wa Togo nchi iliyopo Afrika Magharibi.

Dkt.Slaa ameongeza kuwa kupitia mkatana huo  EU ilikubaliana na nchi za kiafrika kwamba watakuwa na mahusiano kwa kuwa na Bunge la pamoja na nchi za Afrika,Carribean,Pacific na Bunge la Ulaya ambapo Bunge hilo la pamoja  ndio linaloleta hela hapa Tanzania.

“Hela ya bajeti support ilikuwepo tangu mwaka 1975,sasa hatuhitaji popularity ya namna hiyo na tusitafute umaarufu mahali ambako hapako kwa kuonesha kuwa wewe ndiye umefanikisha kuletwa kwa fedha hizo.

“Mimi nimekuwa kwa miaka mitano kwenye Bunge linaloidhinisha hela zinazokuja Tanzania kutokea EU na mimi ni mpinzani ningetaka ningeweza kuzizuia lakini hata siku moja sikufungua mdomo wangu kuzuia kwa sababu hela zile zinakuja nchini kwangu na hii ipo angalieni recods kuanzia 1997”amesema Dkt.Slaa

Akizungumzia  kuanzishwa kwa Bunge la pamoja la nchi za Kusini mwa Afrika SADC,Dkt.Slaa amebainisha kuwa baada ya kuingia bungeni  mwaka 1995 na 1997 alichaguliwa na Bunge la Tanzania kuwa miongoni mwa wabunge wa kwanza wa Tanzania akiwemo Philip Marmo walioenda kuanzisha Bunge la SADC(SADC Parlimentary Forum )  na wakati huo kulikuwa na nchi 12 pekee.

Amesema yeye  na Marmo ndio waanzilishi wa kwanza  wa Bunge hilo na ndio walioshiriki kuandaa Katiba ya kwanza ya SADC kwa kushirikiana na Spika wa Bunge la  Afrika ya Kusini ambaye wakati wa ukombozi aliishi Tanzania na alikuwa mhariri wa gazeti la kwanza la Kiingereza Tanzania baada ya Uhuru na kubainisha  kuwa kitaaluma  alikuwa mwanasheria.

“Kutokana na nafasi hiyo amekaa katika Bunge hilo hadi 2010 na kwa bahati mbaya nilikuwa Mwenyekiti  wa kinachoitwa  Kamati ya Enterparliamentry  Cooperation Committee na hilo lilinipeleka kuzunguka nchi zote 12 za SADC hivyo ninachofanya sio siasa bali ni kwa ajili ya  maslahi ya Taifa na hataacha kupiga kelele”amesema Dkt.Slaa

Next Post
TPA yapongezwa kulinda mazingira

TPA yapongezwa kulinda mazingira

Kinana aingilia kati bei ya pamba,uvamizi wa tembo

Kinana aingilia kati bei ya pamba,uvamizi wa tembo

Dkt.Mpango ataka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) kuvutia washiriki kutoka mataifa mengine

Dkt.Mpango ataka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) kuvutia washiriki kutoka mataifa mengine

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In