• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na Shujaa wa Afrika,

Jenerali Musuguli aliyeongoza majeshi ya Tanzania kumng’oa Iddi Amin wa Uganda atimiza miaka 103

by bajeti
July 25, 2023
in Siasa
0
CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na  Shujaa wa Afrika,

Makamu Mwenyekiti wa Chama Chama Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Mstaafu David Musuguri mwenye umri wa miaka 103 baada ya kumtembelea nyumbani kwake Butiama mkoani Mara Julai 25,2023 ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa shujaa huyo ikiwa ni siku ya Maadhimisho ya Mashujaa. Katikati ni mtoto wa Jenerali Musuguli. (Picha na Fahadi Siraji wa CCM)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,MARA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana ametembelea      Kaburi la Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na kmwelezea kuwa ni mwanamapinduzi wa kweli na shujaa wa Afrika.

Amesema wakati Tanzania ikiadhimisha siku ya mashujaa, Mwalimu Nyerere anabaki kuwa shujaa namba moja wa Tanzania huku pia akimtembelea Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi  na Usalama Mstaafu Jenerali David Musuguri (103) na kumwelelezea kuwa ni alama ya uzalendo wa Taifa, ukombozi na anastahili kuombewa afya njema.

Kanali Mstaafu Kinana ameyasema hayo Julai 25, 2023 baada ya kuzulu Kaburi la Mwalimu Nyerere na kumtembelea Mzee Musuguli nyumbani kwake Butiama mkoani Mara akiwa katika ziara kukagua uhai wa Chama,  utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuzungumza na wanachama.

Akiwa katika Kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na baada ya kuweka shada la maua, Kinana amemwelezea kuwa ni shujaa wa Tanzania na Afrika na kutoa mwito kwa nchi zinazotamani kuzikalia nchi nyingine kiuchumi kuiga mema ya Baba wa Taifa ambaye aliongoza mapambano ya kumaliza udhalimu wa nduli Idd Amin nchini Uganda.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdulrahman Kinana akiwekewa mkono na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Mstaafu David Musuguri mara baada ya kumtembelea nyumbani kwake Butiama mkoani Mara Julai 25,2023 ikiwa ni sehemu ya kumjulia hali na kutambua mchango wa Shujaa huyo.(Picha na Fahadi Siraji wa CCM)

Aidha, akiwa nyumbani kwa Jenerali Musuguri, Kinana alimwelezea kuwa mzalendo wa kweli aliyeongoza mapambano dhidi ya Idd Amin.

“Jenerali Musuguli ameliongoza Jeshi la Ulinzi la Wananchi  wa Tanzania kwa zaidi ya miaka 50, ameliongoza Jeshi katika nafasi mbalimbali, wakati leo tunaadhimisha miaka 44 ya vita ya Uganda Jenerali Musuguri ndiye aliyeyaongoza majeshi ya Tanzania kumng’oa Nduli Idd Amin.

“Jenerali Musuguri ana nishani zote za juu za Jeshi,  nishani zote kubwa za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  ni alama ya shujaa, ni alama ya ukombozi, ni alama ya uzalendo wa taifa letu,” amesema Kinana

Kanali Mstaafu Kinana aliyekuwa ameambatana na viongozi wa Chama na Serikali Mkoa wa Mara kumjulia hali Jenerali Musugul na kuongeza kuwa amefurahi sana kuwa naye ambapo ametimiza miaka 103 ikiwemo kumtakia afya njema

 

Next Post
Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

TPA yapongezwa kulinda mazingira

TPA yapongezwa kulinda mazingira

Kinana aingilia kati bei ya pamba,uvamizi wa tembo

Kinana aingilia kati bei ya pamba,uvamizi wa tembo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In