• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Matukio 1718 ya milipuko na moto hayajachunguzwa

by bajeti
July 24, 2023
in Habari
0
Matukio 1718 ya milipuko na moto hayajachunguzwa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Tanzania (CAG) Charles Kichere

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

UKAGUZI uliofanywa na  Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG) Charles Kichere umebaini kuwa jumla ya milipuko 1,718 ya moto iliyotokea katika mikoa 28 ya zimamoto kwa mwaka 2021/22 haijachunguzwa.

Kifungu cha 5(2c) cha Sheria ya Zimamoto na Uokoaji Na. 14, 2007 kinaipa mamlaka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (FRF) kufanya ukaguzi wa moto ili kupata taarifa zinazohusiana na chanzo cha moto na hasara iliyosababishwa na moto.

Hayo yamebainishwa katika Ripoti ya Mwaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  nchini Tanzania (CAG) Charles Kichere aliyoitoa Machi 29, 2023 kuhusu Ukaguzi wa Serikali Kuu kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Juni 30, 2022

Amesema imebainika kuwa hakuna tukio lolote kati ya matukio hayo ya moto lililochunguzwa, jambo ambalo ni kinyume na Kifungu cha 5(2c) cha Sheria ya Zimamoto na Uokoaji Na. 14 ya mwaka 2007.

Aidha, amesema katika kipindi cha mwaka 2020/21, kati ya milipuko 1,967 ya moto iliyorekodiwa, ni matukio 560 tu yaliyochunguzwa na kusababisha matukio 1,407 ya moto sawa na asilimia 72 kutokuchunguzwa.

“Kwa matokeo haya ukosefu wa uchunguzi unaweza kuzuia uwajibikaji na kuathiri juhudi zinazolenga kuzuia matukio ya moto kwa baadaye.

“Matukio ya mlipuko wa moto na ripoti ya uchunguzi kutofanya uchunguzi wa moto kumesababishwa na uhaba wa watumishi.

“Hii inamaanisha kuwa, sababu za moto hazifahamiki, jambo ambalo linaweza kusababisha ukosefu wa hatua za kuzuia moto na uwezekano wa matukio ya moto kujirudia”amesema CAG Kichere

CAG Kichere amebainisha kuwa kulingana na matokeo ya ukaguzi, anashauri mamlaka husika zichukue hatua kwa kuhakikisha kufuata Kifungu cha 5(2c) cha Sheria ya Zimamoto na Uokoaji Na. 14 ya mwaka 2007, kwa kufanya uchunguzi wa milipuko na matukio yote ya moto yanayotokea ndani ya mikoa ya Zimamoto.

“Kuandaa na kutekeleza mfumo wa kuchunguza matukio ya moto ambayo ni pamoja na miongozo na itifaki za kubaini chanzo cha matukio ya moto na kuchukua hatua stahiki za kurekebisha.

“Kuongeza fedha kwa ajili ya shughuli za uchunguzi wa moto ili kuwezesha mafunzo kwa wachunguzi, ununuzi wa vifaa muhimu,na kuboresha mchakato wa uchunguzi kwa ujumla.

“Kuimarisha uelewa wa wananchi juu ya umuhimu wa kutoa taarifa za matukio ya moto mara moja na kwa usahihi ili kuboresha ubora wa taarifa zilizopo kwa ajili ya uchunguzi”amesema CAG Kichere

Next Post
CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na  Shujaa wa Afrika,

CCM:Mwalimu Nyerere ni Mwanamapinduzi wa kweli na Shujaa wa Afrika,

Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

Dkt. Slaa:Kwa maslahi ya Taifa sitaacha kupiga kelele

TPA yapongezwa kulinda mazingira

TPA yapongezwa kulinda mazingira

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In