• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Wafungwa 3252 ‘waigeuza jela nyumbani’

by bajeti
July 22, 2023
in Habari
0
Wafungwa 3252 ‘waigeuza jela nyumbani’

Waziri wa Mambo ya Ndani Tanzania Mhandishi Hamad Masauni (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) hivi karibuni.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  nchini Tanzania (CAG) Charles Kichere amesema suala la wafungwa kurudishwa tena magerezani bado ni changamoto,baada ya kubainisha wahalifu  3,252 walioachiwa huru kurudishwa tena gerezani.

Amesema suala hilo huenda linachangiwa na sababu mbalimbali ikiwemo kukosekana kwa fursa za ajira pamoja na unyanyapaa katika jamii unaowakabili wafungwa walioachiwa huru.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Mwaka ya CAG Kichere aliyoitoa Machi 29, 2023 kuhusu Ukaguzi wa Serikali Kuu kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Juni 30, 2022 amesema alipitia Ripoti ya Magereza ya mwaka 2021/22 na kubainisha kuwa wafungwa 3,252 wamerudishwa gerezani tena katika kipindi cha mwaka mmoja.

Amesema wafungwa 2,320 wamerudishwa gerezani tena kwa mara ya pili na wafungwa 932 wamerudishwa gerezani tena kwa mara ya tatu na kuongeza kuwa kiwango kisichoridhisha cha kuwabadilisha tabia wafungwa wakati wa kifungo chao kinaweza kuwa sababu kubwa inayochangia hali hii.

“Hii inamaanisha kuwepo kwa gharama kubwa za kuwatunza wafungwa hawa jambo linaloiweka Serikali katika matumizi makubwa ya rasilimali.

“Wahalifu walioingizwa upya magerezani na kufungwa jela mara ya pili ni wanaume 2,261,wanawake 46,vijana chini ya miaka 14 ni 13 jumla ni 2320,hukumu ya kifungo kwa mara ya tatu wanaume ni 924,wanawake wanne na vijana chini ya miaka 14 ni wanne na jumla ni 932 na jumla ya wote wanaume ni 3185,wanawake 50 na vijana chini ya miaka 14 ni 17 na jumla ya idadi ni 3252”amesema CAG Kichere

CAG Kichere amebainisha kuwa Menejimenti ilieleza kuwa inajitahidi kufanya mageuzi makubwa katika mipango ya urekebishaji, na wameandaa na kuwasilisha rasimu ya marekebisho kwa mamlaka za juu.

Aidha ameeleza kuwa kwa sasa wanatoa mwongozo na mafunzo kuhusu programu za kuwarekebisha tabia, kutumia rasilimali zilizopo ndani ya huduma hiyo, na kufanya shughuli mbalimbali kama vile viwanda vidogovidogo, Kilimo, Ufugaji, Ujenzi, Uvuvi na mafunzo ya ufundi stadi katika Chuo cha Ruanda mkoani Mbeya kwa wafungwa wote waliotiwa hatiani.

“Ninapendekeza menejimenti ya Idara ya Jeshi la Magereza kuimarisha utaratibu wa kurekebisha tabia na kuanzisha mipango ya motisha ambayo inaweza kuwa njia bora za kushughulikia tatizo la kurudia vifungo.

“Programu za kurekebisha tabia zinapaswa kuzingatia ujuzi wa ufundi pamoja na kushughulikia sababu za msingi za tabia ya uhalifu kwa wafungwa, kama vile uraibu wa dawa za kulevya au afya ya akili.

“Mipango ya kuwapa motisha wafungwa inaweza kuwahamasisha kushiriki katika mipango ya urekebishaji wa tabia na kuwapa msaada wanaohitaji ili waweze kufanikiwa kuingia tena katika jamii”amesema CAG Kichere

Next Post
Balozi Dkt.Slaa:Bila Muungano Zanzibar isingekuwa salama

Balozi Dkt.Slaa:Bila Muungano Zanzibar isingekuwa salama

Putin aionya Poland

Putin aionya Poland

Dawa za kulevya zadaiwa kuwafanya Papa kuwa na “Wazimu” baharini

Dawa za kulevya zadaiwa kuwafanya Papa kuwa na “Wazimu” baharini

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In