• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Balozi Dkt.Slaa:Bila Muungano Zanzibar isingekuwa salama

by bajeti
July 22, 2023
in Habari
0
Balozi Dkt.Slaa:Bila Muungano Zanzibar isingekuwa salama

Balozi Mstaafu wa Tanzania nchini Swiden Dkt.Willibrod Slaa akizungumza na Mwandishi wa Habari wa Bajeti Communication Goodluck Hongo Julai 19,2023 jijini Dar es Salaam wakati wa mahojiano maalum.(Picha na Mpigapicha wetu)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

TANZANIA haiwezi kulinganishwa na nchi yoyote duniani kutokana na misingi imara iliyoundwa ikiwemo kuanzishwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa,Mgambo na Muungano.

Hiyo ni baadhi ya misingi imara iliyoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye aliona mbali kuliko vijana wengine wanaozungumzia kuvunja Muungano.

Hayo yameelezwa na Balozi Mstaafu wa Tanzania nchini Sweden Dkt.Willibrod Slaa Julai 19,2023 nyumbani kwake jijini Dar es Salaam wakati wa mahojiano maalum na mwandishi wa habari wa Bajeti Communication.

Balozi Dkt Slaa amesema watu wengi hasa vijana hawajui historia ya kuasisiwa  kwa misingi imara ya Taifa hili ambapo hujiunga na siasa za hamasa wakitaka Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uvunjwe.

Balozi Dkt.Slaa ambaye ameiwakilisha Tanzania pia katika nchi za  Denmark, Finland, Norway, Iceland, Estonia, Latvia, Ukraine and Lithuania amesema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliona mbali kabla ya kuasisi na kukubali kuanzishwa kwa mambo muhimu ikiwemo Muungano,Jeshi la Kujenga Taifa na Mgambo.

Akizungumzia kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao ndio umeunda Tanzania amesema bila Muungano Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Abeid Amani Karume asingekuwa salama.

Amesema Tanzania ilikuwa na maadui wengi kutokana na harakati za kusaidia Uhuru katika nchi nyingi za Afrika hivyo bila Muungano hali ingekuwa hatari leo hii.

“Sisi Mwalimu aliona hilo mapema sana,wakati nikiwa Baraza la Maaskofu,(Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC)),Mwalimu alitaka kutembelea taasisi za Kanisa na mara nyingi alikuwa ananiita saa nane usiku ili niweze kumpa dondoo za eneo analokwenda.

“Licha ya kumuandikia na wakati mwingine tunaandika kama hotuba lakini hata siku moja huwezi kusikia amesoma ulichoandika wewe na hali hiyo alikuwanayo Kardinali Rugambwa,sasa siku moja ananiambia Padri,Katibu Mkuu kuna watu wanamdomo mrefu sana wanataka kuvunja Muungano (wakati ule wa G-55).

“Akasema “Kama niko hai sitakubali muungano huu uvunjike na yeyote hata baada ya kifo changu atakayevunja nitamuapiza,nitamuapiza”amesema Dk Slaa

Amesema hakuna Kiongozi yeyote wa Chama cha Mapinduzi  (CCM) atakayekubali  kuuvunja Muungano licha ya kuwepo kwa baadhi ya changamoto.

Amebainisha kuwa hatukuwa wajinga kusaini mkataba wa Muungano ndani ya masaa kwani hata alama za Marekani ziko mpaka leo Zanzibar lakini vijana wanasema kirahisi  kuvunja Muungano kupitia siasa za hamasa.

Amefafanua kuwa watu wengi hawana misingi na ndio wanaojitokeza kutaka kuuvunja Muungano lakini hawajui umuhimu wa suala hilo na misingi yake ya kuanzishwa.

Hata hivyo ameeleza kuwa hakuna Katiba iliyounda Muungano lakini Mwalimu alitoa Dikrii yaani Hati juu ya Muungano ambapo alitoa barua inayoeleza  kinachojulikana kama Tanganyika na itaitwa Tanzania ambapo Kiti cha Zanzibar katika Umoja wa Mataifa kiliondolewa na kikabakia cha Tanzania.

“Ili nchi itambuliwe Umoja wa Mataifa lazima iwe na Kiti Umoja wa Mataifa kama hakuna kiti haiwezi kutambuliwa.

“Wazanzibar wana haki kweli ya kulalamika kwa kupoteza utambulisho wao baada ya muungano lakini wapelekwa polepole bila kuvuragana na ikiwa tutakuja kuvurugana  kitachotokea ni hatari”ameonya  Balozi Dkt.Slaa

Hata hivyo ameongeza kuwa Wazanzibar wanachoumia ni kwamba hawatambuliwi kwa kueleza kuwa wamepoteza utambulisho na kiti Umoja wa Mataifa .

Amesema ni lazima suala hilo lifanywe kwa utaratibu kwani Mwalimu kama asingeingilia Zanzibar Rais Karume asingekuwa salama na wala sio waarabu ndio wangeshughulika lakini Tanzania ilikuwa ndio adui mkubwa wa makaburu na wareno kutoka Msumbuji.

Amesema makaburu walikuwa ndio wanatawala karibu nchi nyingi za Kusini mwa Afrika na Tanzania ndio ilikuwa ikisaidia nchi hizo kupata uhuru.

“Sisi tulimfukuza Mreno pale Msumbiji na  Kaburu alikuwa ndio aliyekuwa na silala akishindana na Ulaya na alitawala karibu kusini kote mwa Afrika sasa kwa Zanzibar  ilikuwa ni dakika tano tu kuingia kwa kuleta meli yake moja tu.

“Sheria za kimataifa zinasema nikikuvamia nikakupiga basi maeneo hayo ni ya kwangu na inabadilisha mipaka na kama makaburu wangefanikiwa kupiga basi eneo hilo lingekuwa la kwao na ndio kinachofanywa na Rais wa Urusi Vladmir Putin”amesema Balozi Dkt. Slaa

Akizungumzia kuhusu Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) amesema watu wengi na vijana hawajui thamani ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa Tanzania na kwa Ukombozi wa Bara la Afrika lakini wao  wanajua.

Amesema tangazo la kuanzishwa kwa JKT lilipotolewa kwa vijana kupelekwa huko walipiga kelele yakiwemo madhehebu ya dini juu ya uamuzi huo wa kuchukua watoto wao kupelekwa jeshini.

Amesema watoto wa kike na wa kiume wote hukaa pamoja ndani ya handaki na kelele zilizopigwa ni juu ya maadili ya kuwaweka pamoja vijana wa kike na kiume kwa kuwa hali ya binadamu inajulikana.

Ameongeza kuwa licha ya kuwa na madhaifu yake JKT lakini vijana waliotoka huko wamekomaa na kujengwa katika utu na kuthamini  na kupelekea wengine kuoana wakiwa makabila tofauti na hata kula chakula wasichokijua na kuwafanya kuwa ndugu.

“Sasa hujui unavyojengwa katika utu wako na kudhamini watu wale na ukatapa mchumba kule Mtwara  sasa hapo watanzania watapigana kweli? Hivi vitu ni vya Tanzania pekee huwezi kulinganisha na nchi yoyote,na vitu hivi havikuja hivihivi tu bali vimeundwa na kwa misingi hiyo Tanzania haiwezi kupigana vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na mifumo kama na nchi zingine duniani.

“Wakati wa vita na Uganda waliotangulia vitani ni JKT na Jeshi la Akiba (Mgambo) sasa vitu hivi ni lazima vijana waelewe msingi wake wasione vyaelea wajue vimeundwa”amesema Balozi Dkt.Slaa

Next Post
Putin aionya Poland

Putin aionya Poland

Dawa za kulevya zadaiwa kuwafanya Papa kuwa na “Wazimu” baharini

Dawa za kulevya zadaiwa kuwafanya Papa kuwa na “Wazimu” baharini

Magonjwa yanayowaathiri  wanyamapori yatajwa

Magonjwa yanayowaathiri wanyamapori yatajwa

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:5
  • Today's page views 5
  • Total visitors 13,061
  • Total page views 14,806

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In