• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

RC Mtaka ataka kutangazwa zaidi fursa biashara ya Kaboni

by bajeti
August 5, 2023
in Mazingira
0
RC Mtaka ataka kutangazwa zaidi fursa biashara ya Kaboni

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka akizungumza na Afisa Mazingira Mwandamizi Ofisi ya Makamu wa Rais Abdallah Lungo (wa kwanza kulia) na Msaidizi wa Mtendaji Mkuu, Habiba Mhina wakati alipotembelea Banda la Ofisi ya Makamu wa Rais katika Maadhimisho ya Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nanenane) yanayoendelea katika Viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya Agosti 4, 2023).(Picha Ofisi ya Makamu wa Rais)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU,MBEYA

MKUU wa Mkoa wa Njombe, Antony Mtaka ameishauri Ofisi ya Makamu wa Rais kuendelea kutangaza fursa za Biashara ya Kaboni ili wananchi wapate ari ya kuhifadhi mazingira kwa kupanda miti hivyo kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Mtaka ametoa ushauri huo Agosti 4, 2023 wakati alipotembelea Banda la Ofisi hiyo katika Maonesho ya Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nanenane) yanayofanyika Kitaifa katika Viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya.

Amesema ni muhimu kutumia vyombo vya habari kuzungumzia manufaa na faida za biashara ya kaboni hususan msisitizo wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango kuhusu faida ya biashara hiyo.

Aidha ameshauri pia iandaliwe programu maalum ya vipindi vya elimu kwa umma vinavyoelimisha wananchi kuhusu fursa, manufaa na mafanikio yaliyopo katika masuala ya Muungano na hifadhi endelevu ya Mazingira.

Ameongeza kuwa vipindi vinavyozungumzia Muungano na Mazingira vina mchango mkubwa katika kuelimisha umma kwani vitawawezesha Watanzania wengi kufahamu msingi na historia ya Muungano pamoja na majukumu mengine muhimu yanayotekelezwa na Ofisi hiyo.

Mtaka amebainisha kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais ni kubwa hivyo majukumu mahsusi inayotekeleza yanapaswa kutambulika na umma, hivyo ni muhimu kuyatangaza kwa kuandaa maudhui ya vipindi na makala mbalimbali zitakazotangazwa kupitia vyombo vya habari vya televisheni, redio na mitandao ya kijamii.

Aidha Mtaka amefafanua kuwa  uaandaji, utengenezaji na urushaji wa vipindi vya elimu kwa umma ni moja ya njia za haraka ya kutangaza shughuli na majukumu ya Wizara ili kuweza kutambulika na kufahamika kwa wadau na jamii.

Hata hivyo Mtaka amevitaka Vitengo vya Mawasiliano Serikalini kuachana na mfumo wa kutumia matukio katika kutoa habari na taarifa kwa umma.

“Yapo masuala muhimu ya kihistoria ya Tanzania ambayo bado jamii ya Watanzania ikiwemo historia ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hatua inayotokana na baadhi ya watu kutopenda kujifunza, hivyo ni wajibu wa Ofisi ya Makamu wa Rais kuzalisha vipindi na machapisho mbalimbali yanayoeleza chimbuko, misingi na historia hiyo“amesema Mtaka

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Antony Mtaka akipokea nyaraka mbalimbali ikiwemo Sera ya Taifa ya Mazingira ya 2021 kutoka kwa Afisa Mazingira Mwandamizi wa Ofisi ya Makamu wa Rais,(wa kwanza kulia) Abdallah Lungo na Msaidizi wa Mtendaji Mkuu, Habiba Mhina mara baada ya kutembelea Banda la Ofisi hiyo katika Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima Duniani (Nanenane) jijini Mbeya Agosti 4, 2023.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Kuhusu elimu ya uhifadhi wa mazingira, Mtaka ameitaka Ofisi hiyo pia kuandaa makala na vipindi vya televisheni na redio zinazofafanua kwa undani dhana na tafsiri halisi ya biashara ya kaboni kwani biashara hiyo kwa sasa ni fursa na mkombozi wa kiuchumi kwa jamii zilizopo katika ukanda wa maeneo ya misitu nchini.

Kwa upande wake Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Abdallah Lungo amemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa kwa maoni na ushauri alioutoa kwa Ofisi hiyo kwa kuwa yatasaidia kuongeza kasi, ubunifu,ufanisi katika kujitangaza zaidi na kuhakikisha kuwa majukumu ya ofisi hiyo yanafahamika kwa wadau na umma kwa ujumla.

Next Post
Wakulima 89,321 mikoa Kanda ya Kaskazini wanufaika na mbolea ya ruzuku

Wakulima 89,321 mikoa Kanda ya Kaskazini wanufaika na mbolea ya ruzuku

Dkt.Bankobeza:Tumieni vikundi  kusomesha wasio na uwezo kupata elimu

Dkt.Bankobeza:Tumieni vikundi kusomesha wasio na uwezo kupata elimu

Jeshi  Niger lakataa amri ya ECOWAS,lapanga safu yake ya uongozi

Jeshi Niger lakataa amri ya ECOWAS,lapanga safu yake ya uongozi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In