• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Wakulima 89,321 mikoa Kanda ya Kaskazini wanufaika na mbolea ya ruzuku

by bajeti
August 8, 2023
in Mazingira
0
Wakulima 89,321 mikoa Kanda ya Kaskazini wanufaika na mbolea ya ruzuku

Meneja wa Kanda ya Kati na Kaskazini wa Kampuni Agricom Africa Peter Temu akizungumza na waandishi wa habari Agosti 6,2023 jijini Arusha juu ya zana mpya za kilimo walizozileta katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Njiro(Picha na Miriam Sarakikya)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MIRIAM SARAKIKYA, ARUSHA

SERIKALI imetoa zaidi ya tani 40,685 za mbolea ya ruzuku kwa mikoa ya Kanda ya Kaskazini inayojumuisha Arusha,Kilimanjaro na Manyara ambapo zaidi ya wakulima 89,300 wamenufaika.

Hayo yameelezwa mwishoni  mwa wiki na Spika wa Bunge la Baraza la  Wawakilishi Zanzibar Zuberi Ali Maulidi wakati akifungua maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini yanayofanyika katika Viwanja vya Njiro jijini Arusha

Amesema katika kipindi cha mwaka 2022/23 Serikali ya Tanzania iliweka nguvu kubwa katika kuboresha Kilimo,Uvuvi na Mifugo ambapo mikoa ya Kanda ya Kaskazini imenufaika na mambo mbalimbali ikiwemo utolewaji wa mbolea za ruzuku kwa ajili ya kuongeza tija kwenye kilimo.

Aidha ameongeza kuwa  kwa mwaka wa fedha 2022/23 jumla ya Tani 17288 zimetolewa kwa Mkoa  wa Arusha na  kuwanufaisha wakulima 19663 .

Mbali na Mkoa wa Arusha,mikoa mingine iliyopokea mbolea hiyo ya ruzuku ni pamoja na Kilimanjaro tani 18557  na kuwanufaisha wakulima 62829 huku Mkoa wa Manyara ukipata tani 4840 na kuwanufaisha wakulima 6829.

“Tunawaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa serikali ili iweze kuendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwani maonesho haya yana lengo la kuonyesha fursa zilizopo katika Sekta za Kilimo,Mifugo na Uvuvi na kutoa elimu kwa wakulima,wafugaji na wavuvi ili uzalishaji wa mazao na bidhaa zinazotokana na sekta hizo uwe na tija na hatimaye kuchangia katika ukuwaji wa uchumi wa nchi”amesema Maulidi

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella amesema  Maonesho ya Wakulima Nanenane yamezidi kuimarika  na kuleta chachu katika sekta mbalimbali hivyo ushirikiano wa kimuungano utaendelea kuleta chachu zaidi kwa wananchi wote wa Tanzania Bara na Visiwani.

Meneja wa Kanda ya Kati na Kaskazini wa Kampuni Agricom Africa Peter Temu,akiwaonesha wakulima (hawapo pichani) aina mpya ya trekta itakayokuwa mkombozi kwa wakulima Agosti 6,2023 wakati wa Maonesho yanayoendelea katika Viwanja vya Njiro jijini Arusha(Picha na Miriam Sarakikya)

Wakati huo huo Kampuni ya  Agricom Africa imetambulisha zana mpya za Kilimo zitakazowasaidia wakulima kuzalisha mazao mengi na kulima kwa kisasa zaidi.

Miongoni mwa zana hizo mpya za Kilimo ni pamoja na trekta aina ya Kubota yenye nguvu(horsepower 75) ambayo inatofautishwa na trekta nyingine zilizopo  sokoni.

Akizungumzia  zana hizo mpya, Meneja wa Kanda ya Kati na Kaskazini wa Kampuni hiyo Peter Temu,amesema uwezo wa trekta hiyo ni sawa na uwezo wa kutumia trekta mbili kwa mara moja ikiwa na na uwezo wa kufanya kazi mahali popote kulingana na aina ya udongo.

Aidha ameongeza kuwa mategemeo yao ni kuwasaidia wakulima wa Kanda ya Kaskazini kuweza kufanya vizuri kwenye kilimo chao ukitengemea trekta hiyo yenye ubora mkubwa kwenye matumizi ya mafuta ,bei inayouzwa hadi katika upatikanaji wa vipuri

Temu amewataka wakulima kutarajia kupata faida kutokana na kile wanachokifanya huku akisema kuwa teknolojia hiyo ni ya kijapani na inasambazwa na  Agricom Afrika pekee ambapo pia hutathimini njia ya kumuwezesha mkulima kuweza kupata faida zaidi kwa kumuinua  kutoka katika matumizi ya zana za zamani na kurudi katika matumizi ya zana za kisasa.

Next Post
Dkt.Bankobeza:Tumieni vikundi  kusomesha wasio na uwezo kupata elimu

Dkt.Bankobeza:Tumieni vikundi kusomesha wasio na uwezo kupata elimu

Jeshi  Niger lakataa amri ya ECOWAS,lapanga safu yake ya uongozi

Jeshi Niger lakataa amri ya ECOWAS,lapanga safu yake ya uongozi

UVCCM yaonya siasa za kukwamisha juhudi za maendeleo

UVCCM yaonya siasa za kukwamisha juhudi za maendeleo

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In