• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Dkt.Bankobeza:Tumieni vikundi kusomesha wasio na uwezo kupata elimu

by bajeti
August 10, 2023
in Habari
0
Dkt.Bankobeza:Tumieni vikundi  kusomesha wasio na uwezo kupata elimu

Wanawake wa Kabila la Wanyambo kutoka Wilaya ya Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera waishio jijini Arusha wakisaga nafaka wakati kwa kutumia mawe wakati wa hafla ya Umoja wao unaojulikana kama Kanono Group jijini Arusha Agosti,2,2023(Picha na Miriam Sarakikya)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MIRIAM SARAKIKYA,ARUSHA

VIKUNDI mbalimbali vinavyonzishwa na makabila yanayoshia nje ya maeneo walikozaliwa wametakiwa kusaidiana katika kudhamini elimu na sio kushiriki katika misiba na sherehe pekee.

Ikiwa vikundi vinavyounda umoja wataamua kusaidiana kwa kuwakopesha au kuwasaidia wale wasio na uwezo wa kusomesha  watoto wao na wanaohitaji kuongeza elimu watawainua zaidi katika maendeleo yao kupitia elimu watakayoipata.

Hayo yameelezwa Agosti 2,2023 jijini Arusha na Mtaalamu wa Sheria Dkt.Gilbert Bankobeza wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya hafla ya Umoja  wa Kabila la Wanyambo unaojulikana kama Kanono Group wanaotoka Wilaya ya Karagwe na Kyera mkoani Kagera waishio mkoani Arusha.

Amesema ni muhimu kwa vikundi kama hivyo vinavyowakutanisha watu wengi wa eneo moja kusaidiana katika masuala ya elimu na sio kusaidiana katika sherehe na misiba pekee.

“Mkisaidiana kwa kuwakopesha au kuwasaidia wale wasio na uwezo wa kusomesha  watoto wao au wale wanaohitaji kuongeza elimu mtawainua zaidi katika maendeleo yao kupitia elimu.

“Watu walio wengi wamekutana katika shule ,vyuo na kuwa marafiki hivyo wakisaidiana katika masuala ya elimu watajenga msingi imara wa elimu kwao na kwa vizazi vijavyo”amesema Dkt.Bankobeza

Wanawake wa Kabila la Wahaya kutoka Wilaya ya Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera waishio jijini Arusha wakitangwa nafaka wakati wa hafla ya Umoja wao unaojulikana kama Kanono Group jijini Arusha Agosti,2,2023(Picha na Miriam Sarakikya)

Kwa upande wake mmoja wa mwananchama wa Kanono Group Erick fidelis amesema kipaumbele kikubwa kitaelekezwa kuwaelimisha vijana umuhimu wa kuenzi na kuendeleza mbinu zilizotumiwa na waasisi wa taifa hili kukabiliana na maovu ikiwemo ya kuimarisha baadhi ya mila na tamaduni  zisizo na madhara

Naye Helen Kazoba amesema mchango wa tamaduni za asili ,mila na desturi  katika kukabiliana na maovu katika jamii ni mkubwa hivyo ni muhimu kuziendelea ili kukabiliana na matendo maovu nayowazunguka vijana na watoto.

Next Post
Jeshi  Niger lakataa amri ya ECOWAS,lapanga safu yake ya uongozi

Jeshi Niger lakataa amri ya ECOWAS,lapanga safu yake ya uongozi

UVCCM yaonya siasa za kukwamisha juhudi za maendeleo

UVCCM yaonya siasa za kukwamisha juhudi za maendeleo

Serikali yaandaa mwongozo Uingizaji, Matumizi na Utupaji Salama wa Zebaki.

Serikali yaandaa mwongozo Uingizaji, Matumizi na Utupaji Salama wa Zebaki.

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In