• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Sayansi na Teknolojia

Vituo binafsi vyaongoza kuwafanyia upasuaji wanawake wanaojifungua.

Mijini waongoza kufanyiwa upasuaji

by bajeti
April 17, 2024
in Sayansi na Teknolojia
0
Utafiti:Watoto walionyonya maziwa ya mama hufaulu zaidi shuleni

Mtoto akinyonya maziwa ya mama yake

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA MWANDISHI WETU

VITUO binafsi vya kutolea huduma za afya nchini vimetajwa kuongoza katika kuwafanyia upasuaji akina mama wanaokwenda kwa ajili ya kujifungua watoto wao tofauti na vya Serikali.

Hata hivyo asilimia 11 ya watoto waliozaliwa hai ndani ya miaka miwili kabla ya utafiti walizaliwa kwa njia ya upasuaji.

Hali hiyo imetajwa katika Utafiti  wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa Mwaka 2022 (DHS-MIS 2022)  uliofanywa na  na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na taasisi zingine ikiwemo Wizara ya Afya.

Utafiti huo umebainisha kuwa njia ya upasuaji inatumika zaidi katika vituo binafsi kuliko vituo vya umma.

‘’Kiwango kikubwa cha kujifungua kwa njia ya upasuaji kinaonekana zaidi maeneo ya mijini kwa asilimia 19 ikilinganishwa na maeneo ya vijijini ambapo ni asilimia nane.

‘’Njia ya upasuaji inatumika zaidi katika vituo binafsi kwa asilimia 30 kuliko vituo vya umma kwa asilimia 12.”umebaini utafiti huo

Mbali na hilo lakini pia utafiti huo umefafanua kuwa kujifungua kwa upasuaji kunaongezeka kadri hali ya uchumi wa kaya inavyoongezeka kutoka kiwango cha chini cha asilimia nne hadi kiwango cha juu cha asilimia 24.

Kwa upande wa huduma za kujifungua,utafiti huo umebainisha kuwa asilimia 81 ya watoto hai walizaliwa katika vituo vya kutolea huduma za afya, kiasi kikubwa cha watoto  ambacho ni asilimia 75 walizaliwa katika vituo vya umma.

‘’Bado ipo changamoto ya watoto wanaozaliwa majumbani ambapo Utafiti huu unaonesha kuwa asilimia 18 ya watoto walizaliwa nyumbani’’umeongeza utafiti huo

Hata hivyo utafiti huo umeonesha  kuwa, kwa ujumla kiwango cha akina mama wanaojifungulia vituo vya kutolewa huduma za afya kimeongezeka katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita kutoka asilimia 52 hadi asilimia 81 na asilimia ya watoto wanaozaliwa nyumbani imepungua kutoka asilimia 47 hadi asilimia 18.

Awali akizungumzia utafiti huo wakati wa semina ya waandishi wa habari kutoka Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC) Mtakwimu Mkuu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Elinzuu Nikodem amesema Utafiti huo umefanyika nchi nzima ikiwemo na  Zanzibar.

Amesema Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Viashiria vya Malaria wa Mwaka 2022 (DHS-MIS 2022) ulilenga kutoa takwimu za kufuatilia na kutathmini hali ya afya ya watu nchini Tanzania.

Amesema Utafiti wa DHS-MIS wa Mwaka 2022 ni wa saba katika mfululizo wa tafiti za kitaifa za kidemografia na afya zilizowahi kufanyika nchini Tanzania tangu mwaka 1991-92.

‘’Lengo la Utafiti huu ni kupata taarifa muhimu kuhusu kiwango cha uzazi, ndoa, kujamiiana, upendeleo wa kuzaa, ufahamu na matumizi ya njia za uzazi wa mpango, unyonyeshaji watoto wadogo, lishe, vifo vya watoto wadogo na vifo vitokanavyo na uzazi,

‘’ Huduma wakati wa ujauzito na huduma za watoto, malaria, na taarifa nyingine zinazohusu afya, pamoja na kiwango cha malaria kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano’’amesema Nikodem

Next Post
Kuelekea Miaka 60 ya Muungano

Kuelekea Miaka 60 ya Muungano

Ushirikiano wa Tanzania na Urusi kuzidi kuimarishwa.

Ushirikiano wa Tanzania na Urusi kuzidi kuimarishwa.

James Mbatia:Asante Mahakama

James Mbatia:Asante Mahakama

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:9
  • Today's page views 9
  • Total visitors 13,065
  • Total page views 14,810

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In