NA MWANDISHI WETU,DODOMA
JESHI la Polisi Tanzania limewataka watanzania wote kuacha kusambaza video katika mitandao ya kijamii zenye kudhalilisha utu wa binadamu kwa kuwa hilo ni kosa kisheria
Kauli ya Jeshi la Polisi imekuja baada ya kunaonekana video inayosambazwa katika mitandao ya klijamii ikimwonyesha binti anayesemekana ametokea eneo la Yombo Dovya Manispaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam akidhalilishwa na kufanyiwa ukatili ambao haukubaliki na ni kinyume cha sheria, maadili ya Mtanzania na Haki za Binadamu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Agosti 4,2024 jijini Dodoma na Msemaji wa Jeshi hilo DCP David Misime amesema kutokana na video hiyo ya udhalilishali utu wa binadamu Jeshi la Polisi limeshaanza kulifanyia kazi tukio hilo ovu na la kulaaniwa.
”Jeshi la Polisi linatoa wito kwa Wananchi wote waache kuendelea kusambaza video hiyo kwani kwa kufanya hivyo ni kosa kisheria lakini pia ni kitendo cha kuendelea kudhalilisha utu wa binadamu mwenzetu.
”Tunatoa wito kwa mwenye taarifa ya kuhakikisha mkono wa sheria unawafikia kwa haraka waliofanya ukatili huu asisite kutusaidia kwa kutupa taarifa au kumpatia kiongozi yeyote yule wanayemwamini kwamba taarifa ikimfikia watu hao watapatikana haraka iwezekanavyo”amesema DCP Misime




Discussion about this post