• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Spika Dkt.Tulia akutana na Rais Sulyok wa Hungary

by bajeti
October 8, 2024
in Habari
0
Spika Dkt.Tulia akutana na Rais Sulyok wa Hungary

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson, akizungumza na Rais wa Hungary, Tamas Sulyok Oktoba 8,2024 katika Ikulu ya nchi hiyo iliyopo Jijini Budapest.(Picha na Bunge)

Share on FacebookShare on Twitter

BUDAPEST,HUNGARY

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson, amefanya mazungumzo na Rais wa Hungary, Tamas Sulyok na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu ushirikiano na amani duniani.

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Oktoba 8, 2024 katika Ikulu ya nchi hiyo iliyopo Jijini Budapest walijadili njia bora za kuimarisha ushirikiano kati ya mataifa haya mawili, Tanzania na Hungary, katika sekta mbalimbali hususani Kilimo, Utalii, Biashara na Maji.

Rais Sulyok alitumia fursa hiyo kumpongeza Dkt. Tulia kwa juhudi zake za dhati katika kuendeleza amani duniani, hususani katika maeneo yanayokumbwa na migogoro mikubwa.

Aidha, walizungumzia pia masuala yanayohusu misingi na malengo ya IPU, ambapo  Rais Sulyok aliahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na kuwa mstari wa mbele katika kuendeleza ajenda zote za IPU.

Ifahamike kuwa kati ya nchi nane zilizounga mkono kuanzishwa kwa IPU katika mkutano uliofanyika Juni 29 na 30,1889 nchini Ufaransa, Hungary ilikuwa miongoni mwao, sambamba na Uingereza, Ufaransa, Marekani, Denmark, Ubelgiji, Uhispania na Liberia kutoka Afrika.

Hii ndio sababu Hungary inaadhimisha miaka 135 ya kuanzishwa kwa IPU.

Next Post
DCEA:Raia wa nchi jirani wanafadhili kilimo cha bangi Mara,yakamata tani 7.8

DCEA:Raia wa nchi jirani wanafadhili kilimo cha bangi Mara,yakamata tani 7.8

Operesheni ya DCEA yasaidia wanakijiji kukataa kilimo cha bangi Tarime

Operesheni ya DCEA yasaidia wanakijiji kukataa kilimo cha bangi Tarime

RC Sendiga ataka uhamasishaji usajili wakulima wanufaike na mbolea za ruzuku

RC Sendiga ataka uhamasishaji usajili wakulima wanufaike na mbolea za ruzuku

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In