• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Tuesday, January 13, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

ACT-Wazalendo kufanya kampeni nchi nzima Uchaguzi Serikali za Mitaa

Wajipanga kufungua kesi kupinga wagombea wao kuenguliwa

by bajeti
November 19, 2024
in Siasa
0
ACT-Wazalendo kufanya kampeni nchi nzima Uchaguzi Serikali za Mitaa

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Dorothy Semu

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

VIONGOZI wa Kitaifa wa Chama cha ACT-Wazalendo wakiongozwa na Kiongozi wake Dorothy Semu wanatarajiwa kushiriki kwenye Kampeni ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji kwenye Mikoa yote ya Tanzania Bara ili kuwanadi wagombea wao.

Akizungumza na waandishi wa habari Novemba 19,2024 mkoani Dar es Salaam,Msemaji, Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa chama hicho Rahma Mwita, amesema kampeni hizo zitaanza Novemba 20 hadi 26,2024 ambapo uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Novemba 27,2024.

Amesema kwenye kampeni hiyo, viongozi hao wa kitaifa watawanadi wagombea wa ACT Wazalendo kwenye vijiiji na mitaa mbalimbali nchini.

Amesema Kiongozi wa Chama hicho Dorothy Semu na Makamu Mwenyekiti Bara Isihaka Mchinjita wataongoza kampeni ya viongozi wa kitaifa kwenye mikoa ya Mkoa wa Kichama Mwambao, Lindi, Mtwara na Mkoa wa Kichama Selous.

Mwita amebainisha kuwa Kiongozi wa Chama Mstaafu  Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake Janeth Rithe na Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Abdul Nondo wataongoza kampeni ya viongozi wa kitaifa kwenye mikoa ya Tabora, Katavi na Rukwa.

‘’Makamu Mwenyekiti Zanzibar Ismail Jussa na Mjumbe wa Kamati Kuu Rehema Ally wataongoza kampeni kwenye Mkoa wa Tanga.

‘’Katibu Mkuu Ado Shaibu na Katibu wa Ngome ya Wazee Janeth Fusi wataongoza kampeni ya kitaifa kwenye Mikoa ya Ruvuma, Iringa, Njombe, Mbeya na Songwe.

‘’Naibu Katibu Mkuu Bara Ester Thomas akiambatana na Naibu Katibu wa Haki za Binadamu Mbarala Maharagande wataongoza kampeni ya viongozi wa kitaifa kwenye Mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Mwanza, Mara, Kagera na Geita’’amesema Mwita

Aidha Mwita ameeleza kuwa Mwenyekiti wa Chama Mstaafu  Juma Duni Haji ataongoza kampeni ya kitaifa kwenye mkoa wa Dar es Salaam ambapo jumla ya mikutano 28 itafanyika.

‘’Mbali na misafara hii, kutakuwa na kampeni itayoongozwa na wajumbe wa Kamati Kuu, Wajumbe wa Halmashauri Kuu na Mawaziri Kivuli kwenye mikoa yote ambayo imebakia.

‘’Kampeni ya viongozi wa kitaifa inakusudiwa kuongeza nguvu kwa kampeni itayofanywa na wagombea katika vijiji, mitaa na vitongoji pamoja na viongozi wetu wa matawi, kata, majimbo na mikoa’’ameongeza Mwita

Katika hatua nyingine,Mwita amefafanuwa kuwa chama chao kimeanza hatua ya kufanya maandalizi muhimu kwa ajili ya kufungua kesi mahakamani kupinga kuondolewa kwa wagombea wao wa vijiji, mitaa na vitongoji.

‘’Ofisi ya Katibu Mkuu imeshakiandikia Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kuomba kuongezewa nguvu ya mawakili kuhakikisha tunafungua kesi dhidi ya kuenguliwa kwa wagombea wote wa vijiji, vitongoji na mitaa’’amesema Mwita

Next Post
Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar ‘aunguruma’ mkoani Katavi

Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar 'aunguruma' mkoani Katavi

Ajali iliyohusisha Bajaji yauwa watu watano Songwe

Ajali iliyohusisha Bajaji yauwa watu watano Songwe

Makumi ya watu na raia wa kigeni wamiminika kuangalia maajabu ya Mti wa Mwalimu Nyerere

Makumi ya watu na raia wa kigeni wamiminika kuangalia maajabu ya Mti wa Mwalimu Nyerere

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:1
  • Today's page views 1
  • Total visitors 13,057
  • Total page views 14,802

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In