• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Thursday, January 22, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Habari

Mkoa wa Mara kinara kilimo cha bangi 2024

Morogoro yashika nafasi ya pili

by bajeti
July 24, 2025
in Habari
0
DCEA:Raia wa nchi jirani wanafadhili kilimo cha bangi Mara,yakamata tani 7.8

Wananchi wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara wakishiriki operesheni ya kutokomeza dawa za kulevya aina ya bangi iliyoendeshwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dwa za Kulevya (DCEA) hivi karibuni(Picha na DCEA)

Share on FacebookShare on Twitter

NA GOODLUCK HONGO

MKOA ya Mara umetajwa kuongoza katika kilimo cha dawa za kulevya aina ya bangi  ikifuatiwa na Morogoro huku Katavi ikishika nafasi ya mwisho kati ya 11 iliyoorodheshwa.

Mwaka 2024 kiasi cha bangi tani 2,303.20 ilikamatwa ambapo mirungi ilifikia tani 18.45

Hata hivyo Mkoa wa Mtwara umeshika nafasi ya tatu kwa kulima dawa hizo za kulevya huku Mkoa wa Iringa ukishika nafasi ya pili kutoka mwisho.

Kwa mujibu wa Taarifa ya Hali ya Dawa za Kulevya ya Mwaka 2024 iliyotolewa Juni,2025 na kuwekwa saini na Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Waziri Mkuu(Sera,Bunge na Uratibu) William Lukuvi pamoja na Kamishna Jenerali  wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)Aretas Lyimo imeeleza  ekari za mashamba ya bangi zilizoharibiwa katika mikoa mbalimbali nchini kwa mwaka 2024.

Katika taarifa hiyo imeonesha kuwa jumla ya ekari 3,045 ziliharibiwa katika Mkoa wa Mara pekee ambapo Mkoa wa Morogoro ukiwa na ekari  1,165 zilizoharibiwa kwa mwaka 2024.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo,Mkoa wa Mtwara ziliharibiwa jumla ya ekari 157 ikifuatiwa na Mkoa wa Arusha ukiwa na  ekari 131 ambapo Mkoa wa Tabora ziliharibiwa ekari 103.

Mikoa mingine ambapo mashamba ya bangi yaliharibiwa ni pamoja na Shinyanga ekari 67,Lindi ekari 35,Dodoma ekari 14,Ruvuma ekari saba,Iringa nne na Katavi ekari tatu.

Hata hivyo bangi imeonekana kuongoza katika kesi zilizofunguliwa katika mahakama mbalimbali nchini ambapo mwaka 2024 pekee jumla ya kesi 850 zilifunguliwa zikifuatiwa na dawa za kulevya aina ya mirungi ikiwa na kesi 340 huku watuhumiwa 7,981 wakikamatwa wakiwemo wa mirungi 1,256

Katika taarifa hiyo mikoa ya Mwanza,Pwani,Kagera,Rukwa,Mbeya,Geita,Dar es salaam,Singida,Manyara,Tanga na Kilimanjaro haikutajwa.

Hata hivyo kukamatwa kwa idadi kubwa ya watuhumiwa kunaonesha ni jinsi gani kazi kubwa inafanyika kutokomeza uhalifu huo ambapo watuhumiwa hao wamekuwa wakitumia njia mbalimbali za kisasa na kisayansi katika kufanikisha biashara hiyo.

 

Next Post
TCRA:Uvumi ndio chanzo kikuu cha vurugu

TCRA:Uvumi ndio chanzo kikuu cha vurugu

Mto Msimbazi ‘waitafuna’ Vingunguti

Mto Msimbazi ‘waitafuna’ Vingunguti

Kamishna Jenerali Lyimo:Tutateketeza dawa za kulevya nchi nzima

Wapakistan vinara biashara dawa za kulevya

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:18
  • Today's page views 18
  • Total visitors 13,277
  • Total page views 15,025

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In