• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, January 18, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

Mto Msimbazi ‘waitafuna’ Vingunguti

Makumi ya nyumba na makaburi yasombwa

by bajeti
August 6, 2025
in Mazingira
0
Mto Msimbazi ‘waitafuna’ Vingunguti

Gari likipita katika barabara iliyoharibika kutokana na mmomonyoko wa ardhi katika eneo la Mtaa wa Butiama uliopo Kata ya Vingunguti jijini Dar es Salaam Agosti 5,2025.(Picha na Goodluck Hongo)

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

ATHARI za kutanuka kwa Mto Msimbazi zimeendelea kuathiri maisha ya wananchi katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam kutokana na makumi ya nyumba kusombwa yakiwemo makaburi.

Hali hiyo inatokana na mmomonyoko wa ardhi katika baadhi ya maeneo ambapo sasa unatishia uhai wa mji wa Vingunguti huku hali hiyo ikiathiri  makazi ya watu na barabara ya kiwango cha lami katika eneo hilo baada ya kingo zake kuendelea kutanuka.

Uchunguzi uliofanywa na Bajeti Communication umegundua kuwa athari za Mto Msimbazi katika maeneo ya Kipawa,Ulongoni,Tabata pamoja na Vingunguti ni mkubwa baada ya makumi ya nyumba kuanguka na kusombwa na maji  huku nyingine zikiwa hatarini kuanguka.

Baadhi ya wananchi waliozungumzia hali hiyo,wamesema kuwa katika eneo la Butiama pekee nyumba zaidi ya 60 tayari zimeshaondoka na kupotea kutokana na kutanuka kwa mto huo.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa uliopo Kata ya Vingunguti jijini Dar es Salaam Elvis Bwahama akizungumza na mwandishi wa habari kutoka Bajeti Coomunication (hayupo pichani) Agosti 5,2025 kuhusu hali ya Mto Msimbazi.

Akizungumzia hali hiyo,Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Butiama uliopo katika Kata ya Vingunguti jijini Dar es Salaam Elvis Bwahama amesema atahari za mto huo ni kubwa lakini wanaishukuru Serikali kwa kumpeleka mkandarasi ambaye atasafisha mto huo na kujengea kingo zake kwa pande zote za mto huo.

Pikipiki la magurudumu matatu(Toyo) likipita katika eneo lililoathiririka na mmomonyoko wa udongo katika Mtaa wa Butiama Kata ya Vingunguti jijini Dar es Salaam kutokanana Mto Msimbazi kutanuka kingo zake hadi kwenye makazi ya watu.

 

Amesema mbali na nyumba kubomoka lakini pia makaburi nayo yamekumbwa na athari hiyo hali iliyoifanya Serikali kuyahamishia katika maeneo mengine.

“Makaburi nayo mengi yaliondoka lakini Serikali ilikuja na mkakati wa kuyahamisha makaburi na mengine yamebakia na mengine yamepelekwa maeneo ya Kinyerezi,lakini ni ukweli nyumba nyingi ziliondoka”

“Sababu kubwa ya huu mto kutanuka ni uchimbaji wa mchanga lakini pia mto huu haujanyooka,yaani unahama (Zigzag) katika pia hata wananchi waliojenga makazi yao bondeni pia wanasababisha  huu mto kuleta uharibifu”amesema Bwahama

Bwahama ameongeza kuwa awali walijaribu kuweka taka katika kingo za mto huo lakini hazikusaidia chochote na sasa wamezuia na pindi wanapowakamata wananchi wanaomwaga taka hizo wanakamatwa na wengine wanalipishwa faini pamoja na kufikishwa mahakamani.

“Kwa sasa kuna nyumba kama saba ambazo zimefanyiwa tathmini ili kuhamisha barabara hiyo iliyomeguka lakini pia kuna mradi wa uboreshaji wa Mto Msimbazi kutoka Benki ya Dunia nayo tunasubiri lakini pia kuna mkandarasi ambaye tayari ameshapatikana.

“Awali mkandarasi alijenga gati na zilisaidia zaidi na sasa atajenga gati mitaa yote ambayo imepitiwa na Mto Msimbazi.

“Pamoja na juhudi ambazo Serikali imezifanya bado tunaendelea kuiomba kwa jicho la huruma waendelee kutusaidia kutekeleza hili jambo kwani wananchi wanaathirika nyumba zao zinaondika hivyo tunaomba watupe kipaumbele kutusaidia kwa kuuboresha huu mto”amebainisha Bwahama

Next Post
Kamishna Jenerali Lyimo:Tutateketeza dawa za kulevya nchi nzima

Wapakistan vinara biashara dawa za kulevya

Spika Mstaafu Job Ndugai afariki

Spika Mstaafu Job Ndugai afariki

ADA-TADEA yataja sababu za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 kuwa huru na haki

ADA-TADEA yataja sababu za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 kuwa huru na haki

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:23
  • Today's page views 23
  • Total visitors 13,180
  • Total page views 14,926

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In