• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Wednesday, May 6, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Siasa

CHAUMMA yataka mfumo wa serikali tatu

Kurudisha kikokotoo cha zamani kwa wastaafu

by bajeti
October 1, 2025
in Siasa
0
CHAUMMA:Hatma ya maisha ya watanzania ni Oktoba 29,2025

Mgombea Urais Kupitia Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mwalimu Salum Juma akiwasili mkoani Geita Septemba 16,2025 ili kuomba wananchi wakichague chama hicho wa kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,225.

Share on FacebookShare on Twitter

NA MWANDISHI WETU

CHAMA Cha Ukombozi wa Umma(CHAUMMA)  kimesema katika siku 100 za kwanza kuingia madarakani kitaweka utaratibu wa mfumo wa Serikali tatu katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbali na hilo lakini pia CHAUMMA itawasilisha bungeni Mswada wa Marekebisho ya Sheria kwa ajili ya kuondoa utaratibu  uliowekwa na sheria w Kikokotoo na kurudisha wa zamani.  

CHAUMMA imebainisha hayo kupitia Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030 iliyotiwa saini na Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwalim Salum Juma ikielezea mfumo wa utalawa ambapo kitajikita katika kuheshimu mgawanyo wa mihimili ya dola  kwa mujibu wa Ibara ya 4(2)  ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kwa kuhakikisha kwamba mihimili ya dola yaani Serikali,Bunge na Mahakama inatekeleza majukumu yake bila kuingilia.

Hata hivyo CHAUMMA imebainisha kupitia Ilani yake kuwa inaamini katika mfumo wa Serikali tatu  yaani Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar

“Katika siku 100 za kwanza za utawala ,CHAUMMA itahakikisha kwamba inaweka utaratibu wa kuanzisha mchakato wa kuandikwa  kwa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ambapo utaratibu wa  mfumo wa Serikali tatu utawekwa rasmi katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania “imebainisha Ilani hiyo.

Kwa upande wa watumishi wa umma,Serikali ya CHAUMMA  itahakikisha kuwa katika siku 100 za kwanza madarakani inawasilisha Bungeni muswada wa marekebisho ya sheria  kwa ajili ya kuondoa utaratibu uliowekwa na sheria wa Kikokotoo

“Tutarejesha utaratibu na  fomula ya zamani ili kuwawezesha watumishi wa umma wanapostaafu kuweza kuanza maisha mapya badala ya mfumo wa sasa unaowalazimisha watumishi kulipwa kidogo kidogo mafao yao jambo ambalo linapelekea wastaafu wengi kushindwa kupanga maisha mapya baada ya kustaafu utumishi wa umma”imeeleza Ilani hiyo

Ilani hiyo pia imeongeza kuwa kwa watumishi wa umma ambao wanastahili kupandishwa madaraja ,Serikali ya CHAUMMA itahakikisha kuwa inawapandisha madaraja kwa wakati na kuwalipa stahiki zao katika muda muafaka ili kuwaondolewa manung’uniko wakiwa kazini.

  “Ilani hii ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025-2030 imejengwa kwa dhati ya kutatua na kumaliza kero zote zinazoukabili umma wa watanzania.

“Ni dira ya maendeleo makubwa yenye lengo la kushika dola ili kufanikisha malengo ya chama chetu kujenga Tanzania yenye uongozi wa maadili,uchumi shirikishi  na jumuishi,jamii yenye haki sawa ,na Taifa lenye maendeleo endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo”imefafanuwa Ilani hiyo.

Watanzania wanatarajiwa kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025 na kumchagua Rais,Wabunge na Madiwani wataohudumu kwa muda wa miaka mitano hadi 2030 ambapo vyama 18 vinashiriki.

 

 

Next Post
CCM kukamilisha mchakato wa Katiba Mpya

CCM kukamilisha mchakato wa Katiba Mpya

Serikali ya ADA-TADEA kuwalipa askari walioshiriki vita vya Kagera

Wanafunzi elimu ya juu kupigwa marufuku kupanga vyumba mtaani

Wamiliki wa  nyumba kuzuiwa kujenga frame za maduka katika maeneo ya makazi

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:13
  • Today's page views 17
  • Total visitors 16,092
  • Total page views 18,257

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In