• About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact
Sunday, May 24, 2026
  • Login
Bajeti
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo
No Result
View All Result
Bajeti
No Result
View All Result
Home Mazingira

‘Majangili’wauwa Wanyamapori  577,Hifadhi ya Taifa Serengeti yaongoza  kwa vifo

by bajeti
May 24, 2026
in Mazingira
0
JET  yawataka waandishi wa habari kujikita katika uhifadhi wa maliasili,mapito ya wanyamapori(Shoroba)

Tembo wakiwa katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha(Picha na Goodluck Hongo)

Share on FacebookShare on Twitter

 

NA GOODLUCK HONGO

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere amebaini matukio ya uwindaji haramu kuwa  yamesababisha  vifo vya wanyamapori 577 huku Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiongoza kwa vifo 325 sawa na asilimia 56 ya vifo vyote vilivyotokea katika hifadhi.

Hayo ameyabainisha katika Ripoti Kuu ya Mwaka ya Ukaguzi wa Mashirika ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 iliyotolewa tarehe 30/3/2026

Amesema Ukaguzi wa Taarifa ya Mwaka ya Utekelezaji wa Kimkakati ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa za Tanzania ya mwaka 2024/25 iliyohusu Hifadhi za Taifa 10 yalibainika matukio 1,962 ya uwindaji haramu ambao ulisababisha vifo vya wanyamapori 577.

“Hali mbaya zaidi ilikuwa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, ambapo matukio 186 ya uwindaji haramu yalisababisha kuuwawa  kwa   wanyamapori 325, ikiwa ni asilimia 56 ya vifo vyote vya wanyamapori katika Hifadhi 10 za Taifa”amesema CAG Kichere

Katika ripoti hiyo CAG Kichere amebainisha kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu  431  na idadi ya vifo vya wanyamapori  39 ambapo  Hifadhi ya Taifa Tarangire ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu  tisa na  idadi ya vifo vya wanyamapori  ilikuwa ni 11.

“Hifadhi ya Taifa Saadani ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu   109 na idadi ya vifo vya  wanyamapori  56,  Hifadhi ya Taifa Mikumi ilikuwa na  matukio ya uwindaji haramu  87 na  idadi ya vifo vya wanyamapori 21.

“Hifadhi ya Taifa Ruaha ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu 436 na idadi ya vifo vya   wanyamapori   50 ,Hifadhi  ya Taifa SerengetI ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu  86 na idadi ya vifo vya wanyamapori  325.

“Hifadhi ya Taifa Katavi ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu  135 na idadi ya vifo vya wanyamapori  0,Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu  77 na idadi ya vifo vya wanyamapori 0 na Hifadhi ya Taifa Arusha ilikuwa na matukio ya uwindaji haramu  44  na idadi ya vifo vya wanyapori 10”amefafanuwa CAG Kichere

CAG Kichere amebainisha kuwa jumla ya matukio ya uwindaji  haramu  ni  1,962  na  idadi ya vifo vya wanyamapori ni 577.

Hata hivyo CAG Kichere hajataja aina ya wanyamapori waliouawa katika hifadhi hizo.

 

Discussion about this post

Contact us:

BAJETI COMMUNICATION

info@bajeti.co.tz
bajetinews@gmail.com
+255718699828
P.o.BOX 18133,
DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Category

  • Habari
  • Magazeti
  • Makala
  • Mazingira
  • Michezo
  • Picha
  • Sayansi na Teknolojia
  • Siasa

Our Visitors

  • Today's visitors:65
  • Today's page views 72
  • Total visitors 16,453
  • Total page views 18,664

Kuhusu Tovuti Hii

Hii ni tovuti ya habari iliyojikita katika kuandika  habari za kina   zikiwemo za mazingira kwa lengo la kuelimisha na kuuhabarisha umma.

Subscribe

  • About
  • Advertise
  • Privacy & Policy
  • Contact

© 2025 Bajeti

No Result
View All Result
  • Home
  • Habari
  • Siasa
  • Mazingira
  • Magazeti
  • Makala
  • Picha
  • Michezo
  • Matangazo

© 2025 Bajeti

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In