NA MWANDISHI WETU
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere amebaini kuwa katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha kuna vyummba 204 havitumiki
Hayo yamebainika katika Ripoti Kuu ya Mwaka ya Ukaguzi wa Mashirika ya Umma ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 iliyotolewa tarehe 30/3/2026
“Nilibaini kuwa vyumba 204 vya ofisi, vyenye mita za mraba 3,087 kati ya mita 12,000 zinazomilikiwa na Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha, vilibaki vitupu na havikuweza kutumika kwa mwaka mzima.
“Jambo hili lilisababisha hasara ya mapato takribani shilingi milioni 666.79 kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni 2025 na hali hii inatokana na ukosefu wa matengenezo ya kutosha wa majengo ya ofisi”amesema CAG Kichere
CAG Kichere amebainisha kuwa vyumba hivyo ambavyo havitumiki vitaisababishia taasisi hasara kutokana na kutokupatikana kwa mapato ya kodi na ongezeko la gharama za matengenezo kwa sababu ya ucheleweshaji wa ukarabati.
“Ninapendekeza kuwa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha kiandae na kutekeleza mkakati wa kupangisha ofisi zilizo wazi na pia, kifanye ukarabati wa majengo ya ofisi ili kuvutia wapangaji.”amesema CAG Kichere


Discussion about this post